Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, October 9, 2012

UWINDAJI PANYA CHANZO CHA UHARIBIFU WA MAZINGIRA


UWINDAJI wa panya (Kacheko kwa lugha ya Kifipa) na wanyama wengine wadogo wadogo kwaajili ya kitoeo umetajwa kuwa miongoni mwa mambo yanayochangia kuchomwa kwa misitu katika kata ya Sintali wilayani Nkasi mkoani Rukwa.

Mmmoja wa wakazi wa kata hiyo Sabasi Severino Mafua ameeleza hayo alipokuwa akichangia mada kwenye mdahalo wa Mabadiliko ya Tabia ya Nchi uliofanyika katika kata hiyo jimbo la Nkasi kusini ulioandaliwa na mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali wilayani hapa (Nkangonet) ukiwa umedhaminiwa na shirika la The Foundation For Civil Society.

Mafua amesema kwa sehemu kubwa kuchomwa kwa mapori kunakofanyika kwenye vijiji vya kata hiyo kunatokana na wakazi kutafuta kitoeo aina ya panya na wanyama wengine wadogo ambao unapochoma msitu ndipo urahisi wa kuwakamata ama kujua wanakojificha unakuwepo.

“Wengi wanachoma ili wapate kitoeo aina ya panya maana ni desturi ya wakazi wa kata hii na wafipa kwa ujumla kula panya kama kitoeo.Na hata ukienda vilabuni utakuta wamechomwa na wanauzwa kwa bei tofauti tofauti.Sasa wachimbaji wa panya hao hulazimika kuchoma mapori ili iwe rahisi kuwakamata.Vivyo hivyo na tuwanyama twingine tudogo tunatopatikana kwenye mapori na vichaka kama panya” anasema.

Sunday, October 7, 2012

HATARINI KUPATA KIPINDUPINDU

WAKAZI wa kata ya Mtenga wilayani Nkasi mkoani Rukwa wapo hatarini
kupata magonjwa ya milipuko ikiwemo kipindupindu kutokana na kuendelea
kutumia maji yasiyo safi wala salama.

Hali hiyo inatokana na uhaba mkubwa wa maji unaovikabili vijiji vya

kata hiyo ambapo sasa wanalazimika kunywa maji yanayochotwa kwenye
madimbwi yanayotumiwa pia na mifugo ikiwemo ng’ombe.

Hatari zaidi ni pale ambapo tayari vijiji kadhaa vilivyopo jirani na

kata hiyo kemeripuka ugonjwa wa kipindupindu na tayari hatua kadhaa
zinachukuliwa na serikali ya wilaya kuhakikisha ugonjwa huo hauenei
kwenye maeneo mengine.

Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Mtenga Angelina Ndotela alisema

wanalazimika kutembea umbali mrefu wa takribani kilometa tatu kufuata
maji kwenye madimbwi yaliyopo kwenye mbuga ambapo pia ndiko wafugaji
hunywesha maji mifugo yao.

“Kwa sasa tunaishi kwa kudra za mwenyezi mungu.Maana maji tunayotumia

kwakweli kikizuka kipindupindu hapa kama tunavyosikia kwenye vijiji
vya jirani sijui kama tutapona.”alisema Ndotela.

Alisema hali hiyo imegeuka neema kwa baadhi ya wakazi hususani vijana

ambao wamekuwa wakitumia pikipiki na baiskeli kuyafuata maji hayo na
kasha kuwauzia wakazi wenzao kwa shilingi 500 kila lita 20.

Kwa upande wake kaimu mwenyekiti wa kijiji hicho Alexanda Kapele

alikiri kijiji kukabiliwa na uhaba mkubwa wa maji hali inayolazimu
wakazi kutembea umbali mrefu kuyafuata maji yasoyo safi wala salama
kwa matumizi ya binadamu.

Naye afisa mtendaji wa kijiji cha Mtenga anayekaimu pia nafasi ya

afisa mtendaji wa kata Daniel Kalumbilo alisema uhaba wa maji katika
vijiji vya kata hiyo unatokana na ukame uliopo uliosababishwa na ujio
wa wafugaji wa kabila la kisukuma ambao wamepeleka idadi kubwa ya
mifugo kupita uwezo wa eneo lililop

Wednesday, October 3, 2012

AJALI ILIYOUA WATU 10 MBEYA



HILI NDILO GARI T 671 ABM TOYOTA HILUX (RANGER) ALILOKUWEMO MBUNGE MARY MWANJELWA LIMETEKETEA LOTE KWA MOTO

PICHA NA MBEYA YETU NA KALULUNGA BLOG





A
UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firauni huo ndio msemo pekee ambao naweza kuutumia katika kukujuza yaliyotokea katika ajali mbaya ya Mbalizi Mbeya Vijijini.

Wakati wengine wakiendelea kuokoa majeruhi wengine wamejikuta wakifanya tofauti na vile ilivyotegemewa pale kijana mmoja alipojitoa mhanga na kuingia katika mmojawapo wa waokoaji na kutaka kumchomolea fedha “ waswahili huita mshiko”.

Asalale kijana huyo ambaye hajafahamika jina mpaka mauti yanamkuta katika tukio hilo alikwidwa na mashuhuda wa ajali hiyo na kupewa kichapo cha mbwa mwizi wa kuku.
Kwa hisani ya blog ya malafyaleleo
Mkuu wa mkoa Mbeya Abas Kandoro akiangalia ajali iliyotokea Mbalizi Mbeya

  Hiace nambari T 587 AHT ikiwa imeharibika kabisa baada ya kugongwa na Lori na kisha kupinduka na kusababisha kifo cha abiria kadhaa akiwemo Askari wa Jeshi la Polisi PC Samson
Lori nambari T 814 BTC na tela nambari T 911  BUV likiwa limeteketea kwa moto baada ya kupinduka

Habari na Ezekiel Kamanga.
Baadhi ya watu waliioshuhudia ajali hiyo, walisema kuwa lori hilo la mafuta lilifeli breki na kuanza kutelemka kwa kasi katika mlima huo, ambapo liliyagonga magari matatu ukiwamo Hiace yenye namba za usajili T 587 AHT.
Kwa upande wake, Muuguzi wa Hospitali ya Ifisi, Sikitu Mbilinyi  alisema mbunge Mwanjelwa analalamika zaidi maumivu katika sehemu ya mgongoni  na miguu  sawa na dereva wake ambaye naye analalamikia miguu na amepasuka sehemu ya kichwani na kubainisha kwamba wamepokea maiti mbili.
Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Abbas Kandolo ametoa taarifa rasmi baada ya kutembelea Hospitali za Rufaa na Ifisi na kusema kuwa watu 10 wamefariki dunia na watu 25 wamejeruhiwa na kwamba 17 wamelazwa Rufaa na wanane wamelazwa Ifisi pia maiti nane zipo Rufaa na mbili Ifisi.
Mkuu huyo wa Mkoa ametoa wito kwa wananchi kufika katika Hospitali hizo ili kutambua maiti na majeruhi na amewashukuru wauguzi kwa huduma nzuri na Jeshi la zimamoto na Polisi kufika kwa wakati katika tukio hilo.

 HIVI NDIVYO MAAFA YALIVYO
 HIVI NDIVYO HILI GARI LILIVYO UNGUA MOTO BAADA YA AJALI
 MAMIA YA WATU WALIOFIKA KUSHUHUDIA AJALI HIYO MBALIZI
 HIVI NDIVYO GARI HILI LILIVYO PINDUKA NA KUWAKA MOTO BAADA YA AJALI
 HII NI GARI NYENGINE AMBAYO PIA ILIWAKA MOTO BAADA YA KUGONGANA 
 FIRE WAKIWA WAMEWAHI ENEO LA TUKIO KWA AJILI YA KUZIMA MOTO HUO
 ASKARI WA USALAMA WA BARABARANI WAKIWA WAMEFIKA ENEO LA TUKIO AMBAPO MAGARI HAYO YAMESABABISHA VIFO VYA WATU 10
 WATU WAKIWA WAMEONGEZEKA KUSHUHUDIA TUKIO HILI LA AJALI
 HUU NDIO MUONEKANO WA GARI HILI LIKIWA LIMEUNGUA LOTE
 HAYA NI MABAKI YA GARI HILI AMBALO NALOLILIUNGUA LOTE
WANANCHI MBALIMBALI WAKIWA WANASHUHUDIA AJALI HUKU WENGINE WAKIWA WANAENDELEA KUOKOA WALIOPATA AJALI
KIKOSI CHA FFU NAO WALIKUWEPO SAMBAMBA KATIKA KUHAKIKISHA ZOEZI LA UOKOAJI LINAENDA KIKAMILIFU.
PIA KATIKA ENEO HILI  MBUNGE WA VITI MAALUM MH.MARY MWANJELWAALIKUWEPO NDANI YA PICK UP ILIYOUNGUWA MOTO, KATIBU WAKE ATEKETEA KWA MOTO HUO.
PICHA  NA HABARI : MBEYA YETU BLOG

utumikishwaji watoto



 Mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya msingi Mapogoro iliyopo wilayani Chunya Lusia Mawazo(10) akiwa amemmeba mdogo wake aitwaye Musa Mawazo walipoungana na wakazi wengine wa kijiji cha Mapogoro kusikiliza hotuba ya balozi wa Denimaki John Fratq alipotembelea mradi wa hifadhi ya msitu iliyopo kijijini hapo.(Picha na Joachim Nyambo)