Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, September 28, 2012

MHANDISI MBEYA KUTIMULIWA KAZI


MHANDISI wa barabara katika halmashauri ya wilaya ya Mbeya Jesse Shengena huenda akawajibishwa kwa kusimamishwa kazi iwapo atashindwa kusimamia ujenzi wa barabaya ya Iwiji-Izyira kwa kiwango cha changarawe katika kipindi cha mwezi mmoja.
             
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro ametoa muda huo leo baada ya kutembelea barabara hiyo yenye urefu wa kilometa sita na kukuta imejengwa kwa kiwango cha vumbi badala ya Changarawe kama mhandisi huyo alivyotoa taarifa kwake na LYAMBA LYA MFIPA imeshuhudia.

Awali mhandisi Shengena alisema barabara hiyo imefanyiwa ukarabati kwa kuwekwa changarawe na kampuni ya Kalambo Civil and Building work ya mkoani Mbeya kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 65 na hadi sasa amekwishalipwa zaidi ya milioni 48.

Hata hivyo mkuu wa mkoa Kandoro hakuridhishwa na ukarabati uliofanyika na kumtaka mhandisi huyo kuhakikisha barabara hiyo inarudiwa kwa kufanyiwa ukarabati kwa kiwango cha changarawe katika kipindi cha mwezi mmoja vinginevyo atawajibishwa kwa kusimamishwa kazi

Monday, September 24, 2012

ASKOFU MKUU DK. MOKIWA ANUSURIKA KUPATA KIPIGO KUTOKA KWA WAUMINI WAKE, AOKOLEWA NA POLISI.

Askofu Mkuu wa Angikana Tanzania,la Dk. Valentino  Mkowa aliyevuliwa kofia ya kiaskofu akiwa chini ya ulinzi wa polisi waliokuwa wamevalia kiraia wakimtoa nje ya Kanisa la Anglikana la watakatifu wote mjini Sumbawanga baada ya kuzuka kwa vuguru kubwa jana.
Mmoja wa waumini wa kanisa la Anglikana la watakatifu wote la mjini Sumbawanga akiwa na jazba wakati wa vurugu zilizoibuka jana mara baada ya kutolewa uamuzi wa nyumba ya maaskofu wa kuridhia  askofu Mathayo Kasagara kuwa kiongozi wao ambapo vurugu kubwa zilizuka na kusababisha askofu Mkuu wa kanisa hilo Dk Mokiwa kuondolewa akiwa chini ya ulizi wa polisi. picha na Mussa Mwangoka
Waumini wa Kanisa la Anglikana la watakatifu wote mjini Sumbawanga jana wakipiga kelele kupinga uamuzi wa nyumba ya maaskofu wa kuridhia  askofu Mathayo Kasagara kuwa kiongozi wao ambapo vurugu kubwa zilizuka na kusababisha askofu Mkuu wa kanisa hilo Dk Mokiwa kuondolewa akiwa chini ya ulizi wa polisi.
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania la Dk. Valentino Mkowa jana amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kunusurika kupata kipigo kutoka kwa waumini wake waliokuwa wenye hasira kali.

Vurugu kubwa ziliibuka mara baada ya kusomwa kwa tamko lililothibisha kuwa nyumba ya maaskofu inamtambua Askofu Canon Kasagara kuwa ni kiongozi wao halali wa kanisa la Anglikana la watakatifu wote Jimbo la Ziwa Rukwa mjini Sumbawanga.

Katibu mkuu wa Anglikana Dk, Dickson Chilongani ndiye aliyesoma tamko hilo mara baada ya kumalizika kwa ibada iliyoongozwa na Askofu Mkuu Dk. Mokiwa.

Akisoma tamko hilo Katibu Mkuu alisema kuwa sehemu ya hoja za msingi kamati ya usimamizi wa kanisa hilo zilidai kuwa uchaguzi uliomweka madarakani Askofu Kasagara uligubikwa na rushwa,si za kweli na nyumba ya maaskofu imeshindwa kuthibitisha hilo hivyo Kasagara ni askofu wao halali.

Kutokana na kauli hiyo waumini hao, walianza kupiga kelele ya kupinga maelezo hayo hali iliyosababisha mjumbe wa Kamati ya kusimamia kanisa hilo Flugence Lusunzu aliposhika kinasa sauti na kueleza kuwa wanao ushahidi wa kutosha kuwa rushwa ilitumika kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi huo uliofanyika zaidi ya miaka miwili iliyopita.

Alidai kuwa uamuzi wa nyumba ya maaskofu haukuwapa fursa ya kusikiliza upande wa walalamikaji ili hali ushahidi upo wazi, kutokana kauli hiyo zilianza fujo zilisababisha askofu Mokiwa kutolewa lugha chafu, kuvuliwa kufia yake ya kiaskofu, huku wengine warusha viti ambavyo alivikwepa hado alipoondolewa akiwa chini ya polisi waliokuwa wamevalia kiraia.

Hali hiyo iliharibu amani iliyokuwa imetawala ndani ya Kanisa hilo ambapo uligeuka kuwa uwanja wa vita huku waumini wakisikika wakidai kuwa ni heri kanisa hilo lifungwe kuliko Askofu Kasagara kuliongoza.

Awali tangu nyakati za asubuhi, polisi waliovaa kiraia walitanda katika viunga vya kanisa hilo ambapo Askofu Mokiwa aliwasili na kurakiwa vizuri na waumini wake waliokuwa wakishangilia kwa nyimbo na mapambio.

Hata hivyo tayari waumini wa Kanisa hilo walionya kwamba askofu Kasagara asikanyage kwenye eneo hilo, kwani kufanya hivyo kunge hatarisha amani onyo ambalo upande wa askofu Kasagara walitii hivyo askofu huyo mwenye makazi yake wilayani Mpanda alibaki katika nyumba moja ya kulala wageni alikokuwa amefikia.

Mmoja wa waumini Julius Michael alisema kwa kuwa waumini wa Jimbo la Rukwa hawamtaki askofu Kasagara hakuna sababu ya kuwalazimishwa lakini nyumba ya maaskofu inapaswa kuangalia uwezekano wa kuligawa jimbo hilo.

Tayari Serikali imegawa mkoa wa Rukwa na kuzaa ule wa Katavi sasa hakuna umuhimu wa kuwalazimisha waumini wampokee mtu wasiyemtaka nyumba ya maaskofu waanzishe jimbo katika mkoa huo mpya na aongoze Kasagara.

Alisema iwapo watatumia nguvu kumuweka Askofu huyo Rukwa haitasaidia kitu kwani hawezi kuwaongoza watu wasiotaka kushirikiana nae.

Mgogoro katika Kanisa hilo umedumu kwa zaidi ya miaka miwili sasa ambapo siku za nyuma waumini hao walimzuia Askofu Mkuu, Dk Valentino Mkowa kumsimika Askofu huyo na badala yake alisikimkwa tarehe 16, Juni mwaka jana Mjini Mpanda.

Kutokana na kujitokeza kwa mgogoro huo, ilifunguliwa kesi mahakamani ya Hakimu Mkazi Sumbawanga na waumini wa anglikana, Fulgence Rusunzu na Rojas Bendera na wenzao 191 yenye namba 11/2011 wakipinga kuchaguliwa kwa askofu Kasagala kuwa kiongozi wa Dayosisi hiyo.

Ambayo iliondolewa baada ya pande mbili zinazovutana kukubaliana kuwa baraza la maaskofu ndilo lenye dhamana ya kutatua mgogoro huo


KWA HISANI YA BLOGU YA PEMBEZONI KABISA

WABAKAJI SASA KUHASIWA

MKAZI wa kata ya Nzovwe,Jijini Mbeya,Rehema Mwamengo (39) amependekeza katika katiba ijayo iwe na sheria ya kuhasiwa sehemu za siri kwa mwanaume yoyote atakaebainika na kuthibitishwa na mahakama kumbaka mtoto wa kike.

Kufuatia pendekezo hilo, umati mzima wa watu uliokuwepo ukisikiliza mkutano huo kuangua kicheko huku wanawake wakionekana kupiga vigelegele na makofi kwa kumsifu mama huyo.

Pendekezo hilo alilitoa mbele ya jopo la wajumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba mpya wakati wa mkutano wa kukusanya maoni toka kwa wananchi juu ya mchakato mzima  wa uundwaji katiba nyingine itakayokuwa imewashirikisha wananchi kote nchini.

Mwamengo alisema kuwa hivi sasa adhabu ya mwanaume anayekutwa na hatia ya kubaka kufungwa jela miaka 30 haitoshi kwa dai kuwa vitendo hivyo bado vinashamili siku hadi siku miongoni mwa jamii.

Alisema kuwa vitendo hivyo licha ya kuwa na adhabu hiyo ya kufungwa miaka 30 jela lakini watoto wanaokuwa wamefanyiwa kitendo hicho hujikuta wakiwa katika hali mbaya ambapo baadhi yao hupata ulemavu sehemu za uzazi.

Aidha, alidai kuwa endapo katiba ijayo itaridhia kuwepo kwa adhabu hiyo ya kuhasiwa kwa mwananume anayekuwa na hatia ya kubaka heshima itakuwepo na itakuwa ni fundisho hata kwa wale wenye tabia ya kupalamia watoto wa kike.

“Nasema hivi mwanaume yoyote atakakaebainika na kuthibitishwa na mahakama kuwa ana hatia hiyo ya kubaka adhabu yake iwe ni kuhasiwa tu ili iwe ni fundisho kwa wanaume wengine”alisema mama huyo na kuongeza:

“Hivi sasa  adhabu ya mwanaume atakaekutwa na hatia kama hiyo kufungwa miaka 30 na adhabu hiyo inatekelezwa na mahakama lakini bado tabia hiyo ipo na inazidi kuwaumiza mabinti zetu, na  hali hiyo  inaashilia kuwa haitoshi kwa mwanaume huyo,hivyo nashauri kwamba adhabu yake iwe ni kuhasiwa tu”alisema.

Sunday, September 23, 2012

RC AKATAA TAARIFA YA MKURUGENZI


MKURUGENZI wa halmashauri ya wialaya ya Mbozi Levison Chilewa amejikuta katika wakati mgumu baada ya mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro kuikataa taarifa yake iliyokuwa ikizungumzia matarajio ya mavuno wakati kipindi cha mavuno kilikwisha malizika.

Thursday, September 20, 2012

YANGA,PRISON ZA

-->
JUMLA ya shilingi 50,436,000 zimekusanywa katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania bara kati ya timu ya Yanga ya Dar es salaam na Tanzania Prison ya jijini Mbeya uliochezwa jumamosi katika uwanja wa Sokoine jijini hapa.

Katibu wa chama cha soka mkoani Mbeya (MREFA) Lawrence Mwakitalu ametangaza makusanyo hayo yaliyopatikana kwa njia ya viingilio kutoka kwa mashabiki 16,812 waliofika kushuhudia mchezo huo.
TUENDELEE KUSUBIRI MAMBO MAZURI YAJA

Monday, September 3, 2012

TAMKO LA IPC JUU YA KUUWAWA KWA MWANAHABARI DAUD MWANGOSI


DIWANI ACHUKUWA FOMU KUGOMBEA NEC


Akizungumza na LYAMBA LYA MFIPA, Sabil alikishukuru chama chake kwa
kuchukua maamuzi ya kurejesha nafasi ya Unec katika ngazi za wilaya
akisema kutasaidia kuijenga CCM zaidi kuwa na wawakilishi kutoka ngazi
hiyo tofauti na kuishia kuwa na mwakalishi ngazi ya mkoa pekee.

Alisema kwa kuwa na uwakilishi wa mkoa pekee kulikibana chama ngazi ya

wilaya kujifunza mambo mengi kupitia mikutano mikuu ya kitaifa hivyo
sasa itakuwa fursa ya kipekee.

Alisema anaamini iwapo atapata nafasi hiyo atakiwezesha chama wilayani

kwake kwakuwa atakapokuwa akizungumza katika mikutano ya kitaifa
ataweza kupeleka pia changamoto za wilayani kwake na hatimaye
kujadiliwa kwa upana zaidi na kutafutiwa ufumbuzi.

“Na pia unapokuwa katika mikutano hiyo kuna mambo unajifunza ya

unapoyaleta kwenu hali inayosaidia kukijenga chama wilayani kwako na
pia unakuwa umekijenga kitaifa.Maana unapozungumzia chama taifa ni
lazima kuwa kinaanzia huku hivyo tunapokuwa na msingi imara huku ndiyo
mafanikio ya kitaifa” alisema.

Sabil ambaye ni diwani wa mwanamke pekee aliyepata nafasi kwa

kuchaguliwa kati ya kata zote wilayani hapa alisema amewahi kuwa
diwani wa viti maalumu na hatimaye akagombea na kuwa wa kuchaguliwa na
sasa anataka nafasi ya Unec.

Hata hivyo alisema si mara yake ya kwanza kugombea nafasi hiyo bali

kupitia mkoa mwaka 2002 aligombea lakini kura hazikutosha na mwaka
2007 pia akagombea hazikutosha lakini zikaongezeka tofauti na mwaka wa
kwanza.

Alisema nia anayo na amechukua fomu akiwa na uhakika wa kushinda

kwakuwa ana imani ataungwa mkono na wanachama wenzake ili awawakilishe
japo kushinda na kushindwa ni matokeo ya uchaguzi.