Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, October 9, 2014

GARIJEMBE SASA SHULE YA WASICHANA MBEYA



SHULE ya sekondari ya garijembe iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Mbeya imeteuliwa na halmashauri hiyo kuwa shule ya wasichana.

Lengo la kuteuliwa kwa shule hiyo kuwa shule ya wasichana ni kuwaepushia adha ya kupatwa magonjwa na mimba zisizotarajiwa wanafunzi wa kike wanaoishi katika nyumba za kupanga wakati wakisoma katika shule mbalimbali za sekondari zilizopo wilayani hapa.

Mkuu wa wilaya ya Mbeya Dk.Sigala amesema baada ya kuliona hilo uongozi wa halmaashauri na wilaya umepitisha maamuzi ya kuiteua shule ya Garijembe kuwa mahali salama kwa wanafunzi wa kike badala ya kujipangia mitaani.
         

Amewataka madiwani kuhakikisha suala hilo wanalipa kipaumbele na kuhakikisha miundombinu inayohitajika inajengwa ikiwa ni pamoja na mabweni ili wanafunzi wa kike waanze kunufaika na mkakati huo.

Amesema uwepo wa shule hiyo itakayowaweka katika mazingira salama wanafunzi wa kike utakuwa ni ukumbusho mzuri pia wa utawala wa madiwani waaliopo hivi sasa kwakuwa watakuwa wameleta mchango mkubwa katika kuinua elimu wilayani kwao.

Amewataka madiwani pia kuhamasisha wananchi kuchangia shughuli za uboreshaji na ujenzi wa miundombinu mipya shuleni hapo ili shughuli hizo zikamilike kwas wakati.

No comments:

Post a Comment