Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, October 21, 2014

WABUNGE WA BUNGE LA CONGRESS LA MAREKANI WATEMBELEA MIRADI INAYOENDESHWA NA ANGLIKANA MBEYA


 
 Mkurugenzi wa Maendeleo wa kanisa la Anglikana dayosisi ya kanda ya Nyanda za juu kusini Padre Jonathan Mwashilindi(kushoto) akitoa maelezo ya namna miradi inayofadhiriwa na Wamarekani


 Wabunge wakikagua bidhaa za mikono zilizotengenezwa na wanavikundi








                                                       HABARI KAMILI

WAJUMBE tisa wa kamati ya bunge la Congres la Marekani wamefanya ziara ya siku moja kutembelea miradi inayoendeshwa na kanisa la Anglikana Dayosisi ya Nyanda za juu kusini inayofadhiriwa na serikali ya Marekani kupitia shirika la Watereed.

Miradi inayoendeshwa na kanisa hilo kwa ufadhili wa wamarekani ni ule wa Kupinga ukatili wa kijinsia(GBV) na ukatili dhidi ya watoto(VAC),Ushauri na upimaji virusi vya ukimwi kwa hiari,Vikundi vya uzalishajimali na mradi wa Elimu ya kuzuia maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi.

Wakiwa jijini Mbeya wabunge hao wamekagua shughuli mbalimbali zinazofanywa kupitia miradi hiyo kupitia hafla fupi ya maonesho iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Mbata kabla ya kurejea jijini Dar es salaam.

Katika hafla hiyo fupi,wabunge hao ambao wameongozana na maafisa wachache kutoka ofisi ya Wizara ya Afya walitaka kujua idadi ya watu ambao wamekuwa wakihudumiwa kupitia miradi inayofadhiriwa na wamarekani na pia namna vikundi vinavyonufaika na miradi hiyo.

Akizungumzia,ujio wa wabunge hao Askofu wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya nyanda za juu kusini John Mwela aliiwashukuru watu wa Marekani kwa upndo wao wa kuendelea kufadhiri miradi yenye lengo la kuistawisha jamii ya watanzania.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Maendeleo wa kanisa la Anglikana dayosisi ya kanda ya Nyanda za juu kusini Padre Jonathan Mwashilindi amesema kanisa limejipanga kuwahudumia watu walio katika hali hatarishi zaidi kwa kuwafikia na kuwapa elimu.

Amesema pia kanisa limejipanga kuimarisha klabu za watu waliopima ambazo uanachama wake haujalishi kuwa mtu aliyekutwa na maambukizi ya VVU au hana ili kuziwezesha kuwa na miradi ya kujiongezea kipato.

Amesema kwa kuziimarisha klabu hizo kutatoa fursa kwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi kuwa na njia za kuimarisha kipato chao na kuondokana na utegemezi.

No comments:

Post a Comment