Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, October 6, 2014

SEMINA YA MAFUNZO KWA WATOA HUDUMA ZA KFW YAFUNGULIWA RASMI



Kaimu katibu tawala mkoa wa Mbeya Bw.Costantine Mushi akitoa hotuba ya ufunguzi wa semina ya siku tatu ya Mafunzo ya watoa huduma wa mradi wa KFW inayofanyika katika kituo cha mikutano cha Mkapa kilichopo jijini Mbeya.
 Watoa huduma wa mradi wa KFW kutoka wilalaya za Ileje,Momba,Mbozi,Chunya na Mbeya jiji wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi


 





 Meneja wa miradi inayofadhiliwa na wafadhili wa NHIF Daud Bunyinyiga akisoma risala ambapo moja kati aliyozungumza na pamoja na mafanikio makubwa ya mradi wa KFW ambapo uandikishaji wa wajawazito umevuka malengo kwa asilimia216.




Kaimu mganga mkuu wa mkoa wa MbeyaPriscar Butuyuyu akizungumza jambo kwenye ufunguzi wa semina hiyo ya mafunzo.


AfisaMawasiliano wa NHIF Luhende Andrew Singu akitoa ufafanuzi zaidi juu ya namna mafunzo yatakavyoendeshwa



Mmoja wa washiri wa semina kutoka wilayani Momba Alisi Msukwa akiwawakilisha washiriki wenzake kutoa neno la shukrani ambapo aliahidi maagizo yaliyotolewa na kaimu katibu tawala watakwenda kuyafanyia kazi kwa ustawi wa jamii wanayoihudumia


Mgeni rasmi akiagana na baadhi ya maafisa wa NHIF ngazi ya taifa na Mkoa kabla ya kuondoka baada ya kufungua semina hiyo.

                         HABARI KAMILI
  
MFUKO wa taifa wa Bima ya Afya(NHIF) umefanikiwa kuvuka malengo ya kuandikisha akina mama wajawazito kupitia mradi wa afya ya mama na mtoto wa KFW kwa asilimia 216.


Lengo la awali la NHIF ilikuwa kuandikisha wajawazito 80,000 katika kipindi cha miaka mitatu ya mradi lakini hadi sasa wajawazito walioandikishwa ni 152,287.

Meneja wa miradi inayofadhiliwa na wafadhili Daud Bunyinyiga amebainisha hayo leo(Oktoba 6) kwenye ufunguzi wa semina ya mafunzo ya siku tatu ya watoa huduma za mradi wa afya ya mama na mtoto(KFW) inayofanyika jijini Mbeya.

Bunyinyiga amesema mafaniko hayo yamepatikana kutokana na ushirikiano mzuri baina ya wafadhili yaani benki ya Maendeleo ya watu wa Ujerumani,NHIF pamoja na watoa huduma kupitia KFW.

Akifungua mafunzo hayo,Kaimu katibu tawala mkoa wa Mbeya Costantine Mushi amewataka wasimamizi wa miradi ya KFW na mfuko wa afya ya jamii(CHF) kuwa wawazi katika utendaji kazi iwao ikiwa ni sambamba na kuweka bayana taarifa za mapato na matumizi ya fedha wanazokusanya.

Mushi amesema kwa kuweka wazi taarifa itaongeza hamasa kwa jamii kuzidi kujiunga na huduma hizo na kunufaika kwa kupata tiba stahili hivyo kuwezesha kuwa na jamii yenye afya njema.



No comments:

Post a Comment