VIONGOZI WA CHADEMA MBEYA MJINI
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema)
kimetoa siku tatu kwa kamanda wajeshi la polisi mkoani humo kukanusha iwapo
hakutoa kauli ya vitisho kwa wafuasi wa chama hicho wakati alipozungumzia
kukataza maandamano yaliyokuwa yafanyike hivi karibuni
Sentensi zenye maneno “Hawa jamaa
nitawafanyia kitu kibaya ambacho hawatokuja kusahau.Niko radhi hata nifukuzwe
kazi” ndizo zinazolalamikiwa na viongozi wa Chadema wanaodai kamanda Msangi alizitamka
alipozungumza na wanahabari.
Katika kikao chao na
wanahabari,viongozi hao wakiongozwa na mwenyekiti wa chama hicho John
Mwambigija na mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi wametoa siku tatu kwa kamanda
Msangi kukanusha kauli hiyo kabla hawajachukua hatua waliyoiita ni ya hatari
zaidi.
Akizungumzia kauli inayolalamikiwa,kamanda
msangi amekana kutamka maneno yaliyochapishwa katika baadhi ya vyombo vya
habari na kubainisha kuwa kwa mtu yeyote anayeijua sheria hawezi kutoa kauli
hiyo.
Aidha Kamanda huyo amesisitiza kuwa
alichosema yeye ni kuwa yeyote atakayeandamana jeshi hilo litamchukulia hatua
kali huku pia akisema yawezekana wapo watu ambao wanataka kulichonganisha jeshi
la polisi na wanachadema kwa kuongeza chumvi katika kauli alizotoa.
No comments:
Post a Comment