Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, October 25, 2014

CHADEMA MBEYA YAPATA PIGO

Mwanzonje akipokea kadi ya CCM kutoka kwa Meya wa jiji la Mbeya Athanas Kapunga.
 Hapa akielezea kinachompeleka CCM akitokea Chadema
 Mstahiki Meya akizungumza jambo baada ya kumpokea

 









CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) Mbeya mjini kimepata pigo kubwa baada ya mmoja wa makada wake nguli kukihama chama hicho na kuhamia Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Kada Machachari aliyekihama Chadema ni Joseph Mwanzonje aliyekuwa Mwekahazina wa chama hicho katika kata ya Iziwa iliyopo jijini Mbeya na alikuwa pia mjumbe wa serikali ya mtaa wa Ilungu uliopo katika kata ya Iziwa.

Akizungumza kabla ya kukabidhi kadi ya Chadema na kukabidhiwa ya CCM,Mwanzonje alisema amechukua uamuzi huo baada ya kuona chama chake hakina mwenendo mzuri.

“Nimefikiri kwa kina nikaona Chadema kila wanachokifanya wanafanya kwa kukurupuka.Hakuna mwelekeo wenye kuonesha dira ya maendeleo ya kichama”

“Maamuzi haya sijakurupuka.Nimefikiri na nikajiridhisha kuwa nahitaji kujiunga na chama chenye mtazamo mzuri.Sijaondoka kwa kificho kwa baadhi ya wanachadema nimewaambia juu ya uamuzi wangu.Naamini pia kati yao wengi watakuja CCM.” Alisema

Akimkaribisha ndani ya CCM mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM mkoa,na mlezi wa Chama hicho tawi la kata ya Iziwa,Mstahiki Meya wa jiji la Mbeya Athanas Kapunga amepongeza uamuzi huo na kumtaka kuwa muadirifu ndani ya chama hicho.

Kapunga alisema kujiunga na CCM ni hatua ya kwanza lakini jambo la pili na lililomuhimu ni kutoa mawazo ya kimaendeleo kupitia vikao mbalimbali vilivyowekwa kwa mujibu wa katiba ya chama.

Alisema yale yote aliyokuwa akiyaona hayatekelezwi na serikali ya CCM katika kuwaletea maendeleo wananchi anapata kuitumia fursa aliyoipata kuwashauri viongozi ili yatekelezwe kwa manufaa ya taifa.

Akiwa ndani ya Chadema Mwanzonje alikuwa tishio kubwa kwa CCM kutokana na nguvu kubwa aliyokuwa akionesha nyakati za kampeni za chaguzi mbalimbali hivyo kujiunga na chama hicho ni faraja kubwa kwa wanaccm katika kukijenga Chama chao.

No comments:

Post a Comment