Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, May 31, 2016

ETI NONGA ANUIA KUIKIMBIA YANGA!AKIRI KIWANGO CHAKE KUWA CHINI!!!

Maneno yaliyowekwa katika ukurasa wa FB wa Yanga yanaeleza hiviiiii......

”Nimeomba kuuzwa na tayari barua ipo mezani kwenye ofisi ya Yanga na nimewatajia mahali ninapopenda kuuzwa, nimeomba kuuzwa ili wasiingie hasara kwasababu walininunua kwa pesa nyingi. Sababu kubwa ya maamuzi Yangu haya ni nafasi finyu ya kucheza niliyonayo katika kikosi cha Yanga kutokana ubora walionao wenzangu wanaocheza nafasi niichezayo na wanatimiza majukumu yao ipasavyo na kuitendea haki nafasi hiyo”, amesema Nonga.

Nonga ameongeza kuwa uamuzi huo ni wakwake mwenyewe na wala hajashurutishwa, ”Maamuzi haya ni yangu binafsi sijashurutishwa na mtu, nafanya hivi ili nijaribu kukinusuru kipaji changu”, aliongeza Paul Nonga.


Je kuna ukweli ndani yakeeee!!!! Na tusubiriii majibu hapa hapa Lyamba Lya Mfipaaaa!

Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa CCM yaanza Mjini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhwavi (wapili kushoto) akikagua jengo la Mikutano la CCM, Dodoma Convetion Centre jana ikiwa ni maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai mwaka huu katika ukumbi huo. Kushoto ni  Ofisa Miliki wa Jengo hilo Tegemeo Saambili. 
Luhwavi akitazama hali ya maua kwenye bustani za jengo la ukumbi huo.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rajab Luhwavi akipata maelezo kutoka kwa Ofisa Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Tegemeo Saambili (kushoto), alipokagua jengo hilo jana Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhwavi akihoji kuhusu hali ya bustani zinazozunguka jengo hilo.
Kaimu Meneja Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Christopher Ngalison akimuonyesha Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi hali ya maua kwenye bustani za jengo hilo, alipokagua jana Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu.
Kaimu Meneja Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Christopher Ngalison akimuonyesha Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi hali ya maua kwenye bustani za jengo hilo, alipokagua jana Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu.
Kaimu Meneja Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Christopher Ngalison akimuonyesha Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi hali ya maua kwenye bustani za jengo hilo, alipokagua jana Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu.
Luhwavi akielekeza namna ya kuboreshwa bustani zinazozunguka jengo la ukumbi huo.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akizunguka jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Cetre, alipokagua jana Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu.
Luhwavi akiingia ndai ya ukumbi wa jengo hilo kuona hali halisi.
Kaimu Meneja Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Christopher Ngalison (kushoto), akimpa maelezo kuhusu hali ya ndani ya jengo hilo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi alipolikagua jana Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu.
Kaimu Meneja Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Christopher Ngalison (kushoto), akionyesha baadhi ya viti ambayo hutumiwa na wajumbe, katika ukumbi huo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi (hayupo katika picha), alipolikagua jana Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu.  Mkuu wa Idara ya Usalama na Maadili Makao Makuu ya CCM, Masudi Mbengula.
Bendera ya Taifa na bendera ya CCM zikipepea kwenye jengo hilo la Mikutano la CCM, kama ilivyo kawaida. 

PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

Mkutano wa Mapitio ya Mpango wa Taifa kwa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi Kipaumbele Wafanyika ARUSHA

Mgeni rasmi wa Mkutano huo Profesa Ayoub Magimba ( kushoto ) akisalimiana na Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu ( NIMR ) Dkt Mwele Malecela ( kulia ), aliyesimama katikati ni Mratibu wa Mpango huo Dkt Upendo Mwingira.
Profesa Ayoub Magimba akisalimiana na Mshauri wa Kitaalamu wa Shirika la RTI  International kutoka Washington DC.
Profesa Ayoub Magimba akifungua Mkutano wa tano wa Mapitio ya Mpango wa taifa wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi Kipaumbele ambao unapitia na kupanga mikakati ya utekelezaji wa kutoa Elimu, kinga na kutibu magonjwa hayo ambayo ni Usubi,vikope,kichocho, minyoo ya tumboni pamoja na matende na Mabusha.
Waratibu wa Mpango huo kutoka halmashauri mbalimbali, wakijiandaa kuwasilisha mada zinazoelezea walivyofanikiwa kutekeleza mipango hiyo kwa mwaka 2015 / 2016, wa Kwanza kulia ni Dkt Mabai Leonard ( Mwanza ), katikati Dkt Faraja Lyamuya ( Dodoma ) na Dkt Ida Ngowi.
Profesa Magimba akiwa katika Picha ya Pamoja na Washiriki wa mkutano huo...

SABABU 10 WAZEE MBEYA KUMUUNGA MKONO JPM

Na Joachim Nyambo.

 
“Kaulimbiu ya Hapa Kazi Tu inatukumbusha kaulimbiu za huko nyuma kama vile Uhuru na kazi,Uhuru ni kazi na Heshima ya mtu kazi”  Ni kauli ya Mwenyekiti wa wazee wastaafu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mbeya,Isakwisa Mwambulukutu wakati wazee hao walipotoa tamko la kupongeza utendaji kazi wa rais John Magufuli.

Tamko hilo liliungwa mkono na wazee wengine wanachama wa umoja huo wakiwemo Edward Ndonde,Daniel Fussi,Kikeke A Kikeke,Rogate Masuba,John Mushi,Bujo Mwakatumbula,Joji Nyirenda,Boniface Kasyunguti,Philimon Mwansasu na mmoja wa waasisi wa TANU mkoani Mbeya,Helena Mwaipasi.

“Sisi wazee tunaounda umoja wa Wazee wa CCM tunaoishi jijini Mbeya kwa niaba ya wazee wenzetu tunapenda kutoa tamko rasmi la kumpongeza rais John Magufuli kwa utekelezaji wake mzuri wa Ilani yetu ya CCM ya uchaguzi ya mwaka 2015 na utendaji wake mzuri wa kazi katika awamu hii ya tano ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”alisema Mzee Mwambulukutu.
 
“Tunapotoa tamko la kumpongeza Dk.Magufuli isieleweke kuwa tunaziona awamu nyingine zilizotangulia hazikufanya mazuri,lahasha.Kama alivyosema aliyekuwa rais wa awamu ya pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi kuwa Kila zama na Kitabu chake,viongozi wa awamu zilizotangulia kila mmoja alifanya mambo kwa kadiri ya karama aliyojaliwa na Mwenyezi Mungu kulingana na hali halisi ya wakati wake huo.Hara Dk Magufuli ni moja ya matunda ya awamu hizo zilizotangulia”anasema.

Mwenyekiti huyu anasema ni Ukweli usiopingika kuwa maendeleo ya mtu au Taifa kwa ujumla hayawezi kupatikana kama watu hawataki kufanya kazi.Ni jambo la kumpongeza rais kwa kuhimiza hilo na anapaswa alisimamie kwa nguvu zote ili nchi iweze kujikwamua kutokana na lindi la umasikini.

Wazee hawa wanasema sababu ya pili ya kumpongeza rais ni Kuimarisha nidhamu na uwajibikaji wa watumishi wa umma.Watumishi wengi wa umma walifikia mahali ambapo walifanya kazi kwa kadiri ya matakwa yao bila kujali taratibu na kanuni za kazi.

“Walisahau ile kauli mbiu aliyotoa rais Ally Hassan Mwinyi isemayo,Usipowajibuka,Ole Wako,Utakumbana na Fagio la Chuma.Sisi wazee tunaamini Magufuli ni fagio la Chuma,kwani matokeo tumeanza kuyaona kwenye sehemu ambazo huduma hutolewa kama vile hospitali,ofisi za serikali na sehemu nyinginezo.”

Sababu ya Tatu ni Kupambana na rushwa,ukwepaji kodi na ubadhirifu wa mali za Umma.Anasema Kwa kwa Kutumbua Majipu,Dk.Magufuli anawakumbusha enzi za Hayati Edward Moringe Sokoine alipopambana na Wahujumu Uchumi.

“Sisi wazee tunamwombea rais Magufuli Mungu amlinde,ili atumbue majipu yote,vipele,chunusi na kukwangua kabisa ukurutu ili Tanzania yetu ibaki safi na yenye afya njema kiuchumi na kiustawi wa jamii”

Kuboresha huduma za jamii ili kuleta hali nafuu ya maisha ya watanzania ni sababu ya nne wanayoitaja wazee hawa kuwasukuma kutoa pongezi zao.Hii ni pamoja na kuboresha huduma hospitalini,kutoa elimu bure toka chekechea hadi kidato cha nne na kuhakikisha mikopo inapatikana kirahisi kwa vijana  wa elimu ya juu.

“Kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara,reli,umeme,maji na mingine mingi hapa anatukumbusha usemi wa It can be done play your part.Hivyo tunatoa wito kwa watanzania wenzetu kutimiza wajibu wao pale walipo ili huduma za kijamii ziweze kuwa bora na kutufanya wote tuwe na maisha nafuu”.

Kufufua na kuhimiza ujenzi wa viwanda ili kuongeza ajira,kuongeza thamani ya mazao yatokanayo na Kilimo,uvuvi na Ufugaji na kuinua uchumi wa Taifa pia limewakosha wazee hawa.Wanasema wameanza kuona matunda kwani mkoni Mbeya tayari kiwanda cha Zana Za Kilimo(ZZK) kimeanza kufanya kazi na baadhi ya vijana wamepata ajira.

“Hapa tukizingatia ile kaulimbiu ya Kupanga ni Kuchagua hakuna kitakachoshindikana.Hivyo tunaomba juhudi ziendelee ili kufufua viwanda vingine kama vile HISoap,kiwanda cha nguo na kiwanda cha kusindika nyama”

Jambo jingine ni Kuboresha na maslahi ya wafanyakazi kwa kuanza na kupunguza kodi itokanayo na mishahara yao kutoka asilimia 11 hadi asilimia tisa.Wanasema wanaamini kutokana na Kutumbua Majipu,kudhibiti wafanyakazi hewa na madeni hewa hali ya kiuchumi itakuwa bora na hivyo kuwezesha kuongezeka kwa mishahara ya wafanyakazi na huduma bora kwa umma zitapatikana.

“Jambo ji ngine ni kuhimiza ujenzi wa Taifa linalojitegemea.Ile kauli ya rais Magufuli ya Bora kushindia mihogo,kuliko mkate wa Siagi wa masimango unatukumbusha kauli ya Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere ya Heri kuwa masikini na Huru,Kuliko kuwa Tajiri na Mtumwa”

“Sisi wazee tunamwomba rais wetu akaze uzi wala asijali vitisho vya wafadhili wanafiki na maneno ya Wanasiasa Uchwara.Tunaamini pia kwa kubana matumizi ya serikali kwa kupunguza safari za nje ya nchi,posho za vikao visivyo na tija kwa taifa letu na kupunguza sherehe zinazomaliza fedha nyingi nchi yetu itaweza kujikwamua kiuchumi na hatimaye kuweza kujitegemea”

Wazee hawa wanasema unyenyekevu aliouonyesha Dk.Magufuli wakati wa kuzindua Daraja la Kigamboni ni wa kipekee.Pamoja na kwamba usimamizi wa ujenzi wa daraja hilo ulikuwa chini yake tangu alipokuwa Waziri wa Ujenzi,alikataa daraja hilo kuitwa jina lake na badala yake aliamua liitwe Daraja la Nyerere,kwa kumuenzi Baba wa Taifa kwa kuimarisha umoja wa Kitaifa na kupigania Uhuru wa Bara la Africa.

Mzee Mwambulukutu anasema Kudhibiti uagizwaji holela wa sukari toka nje ya nchi ili kuhakikisha watanzania wanapata sukari iliyo salama na kwa bei nafuu na pia kukuza viwanda vya sukari vya hapa nchini,inastahili pongezi.Pamoja na purukushani za hapa na pale zinazofanywa na wafanyabiashara wasio na Uzalendo wanaamini juhudi za Rais zitashinda kwakuwa Palipo na Mwanga,giza hujitenga.

“Jambo la mwisho ni kudhibiti hali ya ulinzi na usalama visiwani Zanzibar na hivyo kufanikisha uchaguzi wa marudio bila fujo.Akiwa Amirijeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,aliweza kuhakikisha ulinzi na usalamakatika visiwa vya Zanzibar unakuwepo na hivyo kuwezesha uchaguzi wa marudio kufanyika hapo Machi 20 mwaka hu bila vurugu zozote.”

“Sisi wazee tunampongeza kwa hilo na tunapongeza ushindi wa kishindo wa CCM katika uchaguzi huo,uliofanyika kwa amani na utulivu”alisema Mzee Mwambulukutu.

Wazee wengine akiwemo Kikeke A Kikeke,wanasema juhudi na ushirikiano wa pamoja baina ya watanzania wote pasipokujali nafasi waliyonayo ndiyo utakaowezesha mikakati mbalimbali ya Dk.Magufuli kufanikiwa.iwapo kutakuwepo na makundi ya watu wanayojitenga na kukwamisha itakuwa vigumu kwake kuwezesha watanzania kupiga hatua kimaendeleo.

Kwa upande wa katibu wa umoja huo Philimon Mwansasu,alisema watanzania wanapaswa kutambua kuwa maisha bora hayawezi kupatikana kama taifa litabakia mikononi mwa matajiri wachache wenye kupenda kulimbikiza mali kwaajili yao na familia zao na kuwaacha masikini wakiwa watumwa ndani ya taifa lao.

“Tunachopaswa kufanya watanzania wote ni kushirikia katika mipango ya rais kuhakikisha tunafichua maovu yote yanayofanywa na watendaji wabovu.Kuchukuliwa kwao hatua ndiyo mwanzo wa walalahoi kupata unafuu wa ugumu wa maisha.Tukisema tushirikiane na wahalifu kwa madai kuwa tunawaonea huruma tutakuwa tunazidi kujikwamisha wenyewe”anasema Mwansasu.

Mwisho.

Saturday, May 28, 2016

KUMEKUCHA KIPYE CUP 2016,TIMU 14 KUTEULIWA KUSHIRIKI

MAANDALIZI ya Mashindano ya kuibua vipaji katika soka Wilayani Mbarali mkoani Mbeya ya Kipye Cup 2016 yamezidi kushika kasi ambapo kesho(Mei 29) timu 14 zinatarajiwa kupitishwa ili kushirili mashindano hayo.

Kwa mujibu wa mratibu wa Kipye Cup,Frank Kipye,mashindano hayo ambayo ni msimu wa tatu sasa tangu kuasisiwa kwake yatashirikisha timu 14 ambapo tati ya hizo 10 zitakuwa zikitokea katika kata ya Mapogoro wilayani Mbarali na nne ni kutoka nje ya kata hiyo ili kuleta ushindani.

Akizungumza na Lyamba Lya Mfipa,Kipye amesema kamati ya ligi hiyo kesho itakuwa na kazi ya kupitisha timu 14 kati ya zile zilizochukua fomu kuomba usajiri wa kushiriki mashindano hayo.

Amesema mara baada ya timu shiriki kuteuliwa,kazi itakayokuwa imesalia ni kutangaza tarehe rasmi ya kuanza kwa michuano huku akisisitiza kuwa zawadi kwa msimu huu ni mshindi wa kwanza Ngombe mwenye thamani isiyopungua shilingi milioni 1.5,mshindi wa pili lakini tano,wa tatu laki tatu.

“Lengo la mashindano hayo ni kuibua vipaji vya soka sambamba na kutoa hamasa kwa jamii kupenda michezo kutokana na faida zake nyingi ikiwemo vijana kuepuka matumizi ya dawa za kulevya,ulevi na pia ngono zembe.”

Kipye amesema msimu huu mashindano yanatarajiwa kuwa na mvuto zaidi kutokana na kamati ya maandalizi kuamua kuongeza idadi ya timu kutoka nje ya kata ya Mapogoro.

“Ligi itaendeshwa katika uwanja uliopo Mabadaga kata ya Mapogoro.Tumeona tuongeze timu kutoka nje ya kata ili kuleta mvuto zaidi.Mwaka jana tulishirikisha timu mbili tu kutoka nje ya kata.”anasema Kipye.

Kwa msimu wa mwaka jana bingwa wa ligi hiyo ilikuwa timu ya Kapunga FC ambao mwaka huu wanatarajiwa kuwa mabingwa watetezi.

Thursday, May 26, 2016

NIACHE NISOME YAZINDULIWA RASMI

MKUU WA MKOA WA MOROGORO DR KEBWE STEVEN KEBWE AMEZINDUA KAMPENI YA NIACHE NISOME ILIYOHASISIWA NA MKUU WA WILAYA YA ULANGA YENYE LENGO LA KUTOKOMEZA TATIZO LA MIMBA KWA WANAFUNZI.

AKIZINDUA KAMPENI HIYO ILIYO NA KAULIMBIU YA MAGAUNI MANNE, YENYE TAFSIRI YA SARE YA SHULE, JOHO LA MAAFALI,  GAUNI LA HARUSI NA GAUNI LA MAMA MJAMZITO AU MATENITI, MKUU WA MKOA AMEPONGEZA HATUA HIYO NA KUSISITIZA KUWA ITAINUA KIWANGO CHA UFAULU KWA WANAFUNZI WA KIKE WILAYANI HUMO.

DR KEBWE MARA BAADA YA KUZINDUA KAMPENI HIYO AMEPIGA MARUFUKU USHIRIKI WA WANAFUNZI KATIKA SHUGHULI ZA MUZIKI UNAOPIGWA NYAKATI ZA USIKU MAARUFU KWA JINA LA VIGODORO NA KUMTAKA MKUU WA WILAYA KUWAFUATILIA WANAOHUSIKA KUWAPA MIMBA WANAFUNZI NA KUWACHUKULIA HATUA ZA KISHERIA.

AIDHA KATIKA KUUNGA MKONO KAMPENI HIYO YA NIACHE NISOME MAGAUNI MANNE MKUU WA MKOA DR. KEBWE AMEKABIDHI VITI NA MEZA THEMANINI NA TANO ZILIZOTOLEWA NA KAMPUNI YA UCHIMBANI MADINI YA KIBARAN KWA AJILI YA SHULE YA SEKONDARI YA NAWENGE.

MKUU WA MKOA AMEIPONGEZA KAMPUNI HIYO KWA KUANZA KUONESHA NIA YA KUSAIDIA JAMII KATIKA MASUALA MBALIMBALI YA MAENDELEO, HUKU AKISISITIZA HALMASHAURI KUSIMAMIA MIKATABA NA KUSHIRIKIANA NA WAWEKEZAJI ILI KUONGEA MAPATO YA NDANI YA WILAYA.

MWANDISHI: GEOFREY LIKANGAGA 

Saturday, May 21, 2016

ZIARA YA WANACHAMA WA TAJATI,SUPRISE BEACH MJINI MAKAMBAKO

 Wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji Tanzania(TAJATI) wakipiga picha ya pamoja na mkurugenzi wa kampuni ya Star Entergrated inayomiliki Suprise Beach Bw.Patrick Kyando (aliyeshika kitabu)kabla ya kuanza kutembelea vivutio mbalimbali ndani ya eneo lake.
 Baadhi ya wanachama wa TAJATI wakiwa wamepanda mkokoteni unaokokotwa na Punda kuelekea Suprise Beach.

Mwenyekiti wa TAJATI,Bw.Ulimboka Mwakilili akiwa amepanda Farasi njiani kuelekea Suprise Beach.


 Hapa ni langoni pa Suprise Beach.Ukifika hapa lazima utavutiwa kupiga picha kwaajili ya ukumbusho kama ilivyotokea kwa wanatajati hawa.
 Mwenyeji akitoa maelezo katika eneo ambalo hutumika kwa shughuli mbalimbali ikiwemo sherehe za Harusi.
 Kwa mbaali kulia ni mfano wa Mlima Kilimanjaro na kushoto ni mfano wa boti.Hapa unaweza kujifunza kupanda mlima na pia kupanda boti.


 Wanatajati wakiwa wamepozi katika eneo lililopewa jina la Mwanza.Kimsingi linavutia na unaweza kujihisi kweli umefika jijini Mwanza kutokana na mandari yanayofanana.








 Mwanahabari kutoka TV 1 Laudence Simkonda akipiga kasia alipoamua kucheza na Mtumbwi kabla ya kupata ajali kama inavyoonekana hapo chini.

 Wanatajati wakivuka kutoka eneo la Kigamboni kwenda kisiwani Zanzibar(Haya ni majina tu yaliyowekwa hapa)

 Mwanahabari Felix Mwakyembe(aliyekaa) alikuwa mmoja kati ya wanatajati ambao hawakutaka kuondoka ndani ya eneo hili la kuvutia na la starehe za kipekee.
 Mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Bw.Joachim Daniel Nyambo(Jodany)akionesha umahiri wa kusafiri ndani ya maji kwa kutumia Mtumbwi.

 Mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Bw.Joachim Daniel Nyambo(Jodany)akicheza na nyani mdogo aina ya ngedere aliyepewa jina la King.


 Mwanahabari Laudence Simkonda akiwa ametumbukia kwenye maji baada ya mtumbwi wake kupinduka.Hata hivyo kutokana na uzoefu wake aliweza kujiokoa mwenyewe pasipo hata kuhitaji msaada wa mtu mwingine.

 Mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Bw.Joachim Daniel Nyambo(Jodany) akiendelea na kazi ya kupiga picha za matukio mbalimbali wakati wa ziara hiyo.