Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, May 20, 2016

LAFARGE YAZINDUA SARUJI YA TEMBO FUNDI

Mtendaji Mkuu wa Lafarge Tanzania Ilse Boshof akiwa ameshika mfuko wa saruji aina ya TemboFundi akiwa pamoja na Mkurugenzi wa masoko na mawasiliano


Mkurugenzi wa Masoko na mawasiliano wa Lafarge, Allan Chonjo akizungumza jambo wakati wa hafla ya kuzindua aina mpya ya saruji ya Tembo Fundi

Meneja Mawasiliano wa Lafarge, Straton Bahati akizungumza namna watakavyoweza kuwafikia wateja na kutoa elimu kuhusu matumizi ya Saruji mpya ya TemboFundi.

Kampuni ya Saruji ya Lafarge Tanzania imezindua saruji ya kwanza maalumu kwa matumizi ya uashi.

Saruji hiyo inayojulikana kama Tembo Fundi itawapa wajenzi chaguo bora kwa ajili ya kazi za uashi ikiwa ni pamoja na kupiga plasta ukuta, kusakafia, kujengea tofali na kupangilia marumaru.

Saruji hiyo iliyotengenezwa maalum kwa kazi ya uashi wa kuta za nje na ndani inatajwa kuwa na ubora katika kufanya kazi, nguvu kwenye ugundishaji,inashika vizuri na ina umaliziaji bora wenye kuleta matokeo yaliyo bora zaidi kwenye kujenga tofali, uzio, marumaru na sakafu.

Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Ilse Boshoff, alisema wakati wa uzinduzi kuwa Tembo Fundi imeundwa mahususi kwa ajili ya kazi za uashi na kuwapa wajenzi utendaji bora wa kazi na thamani ya fedha.

 “Ikiwa imetengenezwa kutokana na uzoefu na utaalamu wa Lafarge kimataifa katika kuzalisha saruji, Tembo Fundi ni rahisi kutumia katika kupiga plasta, tofauti na saruji ya matumizi ya jumla ambayo itamchukua muashi muda mrefu katika kusawazisha ukuta.”alisema Boshoff

Boshoff alisema faida nyingine muhimu katika matumizi ya Tembo Fundi ni unafuu katika gharama kutokana na mfuko mmoja wa Tembo Fundi kutumika eneo pana zaidi ukilinganisha na mfuko wa saruji ya matumizi ya jumla.

Kutokana ya kwamba inafanya kazi vizuri na uimara wake kudumu kwa muda mrefu Tembo Fundi itawasaidia wajenzi kupunguza gharama kwa kiasi kikubwa.
 

No comments:

Post a Comment