Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, May 19, 2016

WAREMBO 11 KUWANIA TAJI LA MISS MBEYA

 Washiriki wa shindano la walimbwende la Miss Mbeya City 2016 wakiwa katika pozi wakati wa kikao cha mratibu wa mashindano hayo yatakayofanyika kesho Ijumaa(Mei 20) Tom Chilala na wanahabari.

 Mratibu wa mashindano ya Miss Mbeya 2016 Tom Chilala akifafanua jambo kwa wanahabari waliohudhuria kikao cha maandalizi kilichofanyika katika Hoteli yaBeaco jijini Mbeya



WAREMBO 11 wanatarajia kupanda Jukwaani ijumaa hii(Mei 20) kuwania taji la Miss Mbeya 2016 kwenye mashindano yatakayofanyika katika Hotel ya Paradise,Soweto jijini Mbeya.

Warembo wanaowania taji hilo ni Emmiliana Abdalla,Anitha Patric,Aziza Lysamuya,Praxeda Geofray,Juliana Gilbert,Nancy Matta,Agnes Boliva,Julitha Mponela,Afrodisia Chapa,Eunicer Robert,Priscar Mengi na Juliana Lyampawe.

Mratibu wa mashindano hayo Tom Chilala amesema maandalizi yote yamekamilika na kilichobakia ni warembo kupanda jukwaani mbele ya mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makala atakayekuwa mgeni rasmi.

Chilala amesema kuwa majaji wa shindano hilo akiwemo mwenyekiti wa shindano la Miss Kanda ya nyanda za juu kusini Dosi Magambo ndiyo watakaosimamia vigezo vyote vya kuchagua mshindi.

“Shindano linatarajiwa kuvuta hisia za mashabiki wengi kutokana na muonekano wa warembo wa mwaka huu na pia umaarufu alionao kwa sasa msanii Hamornize atakayepamba onesho hili”

“Awali washiriki walikuwa kumi na tano lakini baada ya kuwachuja wakiwa kambini wamebakia kumi na moja ambao ndiyo watapanda jukwaani kuwania taji”anasema Chilala.

Mratibu huyo amesema mshindi wa kwanza katika mashindano hayo atazawadiwa fedha taslimu shilingi laki saba,wa pili laki nne,wa tatu laki tatu na wan ne laki mbili huku waliosalia wakipewa kifuta jasho cha shilingi 80,000 kila mmoja.

No comments:

Post a Comment