Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, April 19, 2018

TEMBO WAMVAMIA KIKONGWE,WAMJERUHI HADI KIFO


WANYAMA Tembo watatu wamemvamia na kumjeruhi na kimsababishia kifo Kikongwe aliyefahamika kwa jina la Sixbertha Mtundu(88) mkazi wa kitongoji cha Mbuyuni mtaa wa Ihanga kata ya Rujewa wilayani Mbarali

Afisa Mtendaji wa Kata ya Rujewa wilayani Mbarali,John Mpangala amesema tukio limetokea juzi saa 11 za jioni maeneo yaliyopo jirani na Ikulu ndogo ya wilaya ya Mbarali.

Mpangala amesema kikongwe huyo amevamiwa na tembo hao wakati akitokea shambani kwake na inasadikika kutokana na umri wake mkubwa huenda hakuwaona wanyama hao mapema na pia alishindwa kukimbia baada ya kuvamiwa.

Hata hivyo Afisa mtendaji huyo amesema tukio hilo liligunduliwa na msamaria mwema mmoja aliyepita eneo hilo na kukuta kikongwe huyo akiwa amelala njiani huku amejeruhiwa vibaya kwa kukanyagwa na tembo na ndipo mkazi huyo alikwenda kwa mwenyekiti wa kitongoji na kumjulisha na ndipo wakaenda eneo husika ikiwa ni majira ya saa moja na nusu usiku lakini wakakuta amekufa.

Afisa mtendaji huyo amesema walichokifanya baada ya tukio hilo ni kuwapa taarifa wenyeviti wa vitongoji vya maeneo ya jirani ili waweze kuwapa tahadhali wananchi kuwa bado tembo hawajulikani walipo japo njia waliopikuwa wakielekea inakwenda eneo la Hifadhi ya Mpanga Kipengele hivyo huenda wapo au wamekwenda hifadhini.

Amesema eneo la tukio kwa miaka ya nyuma ilikuwa njia(Shoroba) ya wanyama lakini baada ya shughuli mbalimbali za kibinadamu hususani kilimo na makazi kukithiri wanyama hawakuendelea kupita tena.





Tuesday, April 17, 2018

ABIRIA WAKWAMA KWA MUDA WILAYANI CHUNYA


 CHINI-Mamia ya Abiria wakiwa wamelazimika kutoendelea na safari juzi baada ya gari za abiria na mizigo zinazofanya safari zake kati ya jijini Mbeya-Chunya hadi Tabora na Singida kukwama katika kata ya Matundasi wilayani Chunya kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha.




DC MJEMA AONJA ADHA YA MAFURIKO AKIKAGUA ATHARI ZA MAFURIKO ILALA

DC MJEMA AONJA ADHA YA MAFURIKO AKIKAGUA ATHARI ZA MAFURIKO ILALA

 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akisaidiwa kuvuka kwenye daraja la muda alipokuwa akikagua leo daraja la Mto Msimbazi linalounganisha Ulongoni B na Gongo la Mboto, Dar es Salaam, ambalo ni moja ya madaraja yaliyobomoka kutokana athari za mvua za masika zinazoendelea kunyesha. Mjema alifanya ziara ya kukagua miundombinu ya barabara iliyoathiriwa na mvua katika wilaya hiyo. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA KAMANDA WA MATUKIO BLOG 0715264202

 Mjema akimpa pole mmoja wa akina mama aliyevuka katika daraja la hilo  la muda linalohatarisha usalama wa wananchi wanaopita hapo.
 Mkuu wa Wilaya Mjema, akizungumza na wakazi wa Ulongoni baada ya kuwafuata upande wa pili kwa kutumia daraja hilo hatari.

 Mjema akiondoka baada ya kukagua daraja hilo la Ulongoni B.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mjema (kulia) akishauriana na Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Edward Mpogolo pamoja na Mkurugenzi wa Manisapaa ya wilaya hiyo, Msongela Palela alipofika kukagua daraja la Banguo Pugu Mnadani eneo ambalo mto umeacha kupita darajani na kumega eneo la barabara hali iliyosababisha kukata mawasiliano ya usafiri katika eneo hilo.
 Wakiangalia jinsi mto Msimbazi ulivyoacha mkondo wake wa kawaida na kumega ardhi
maeneo ya makazi ya watu pamoja na kuharibu barabara.
 Baadhi ya nyumba eneo la Bangua ambazo zimo hatarini kubomolewa na mafuriko.
 Nyumba iliyozungukwa na mto kila upande.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mjema akioneshwa na mtoto nyumba anayoishi na wazazi wake.
Mtoto huyo alisema kuwa hajaenda shule kutokana na eneo hilo kutokuwa na eneo la kuvuka ng'ambo ya pili iliko shule yao.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mjema akioneshwa mkondo wa maji ambao umezibwa baada ya baadhi ya wakazi wa Majohe, kuuziba kwa kujenga nyumba kwenye mkondo huo kitendo ambacho kimesababisha maji kuingia kwenye majumba ya watu.
 Mjema akiangalia baadhi yanyumba ambazo zimejengwa kwa kuziba mkondo wa maji eneo
la Majohe, Dar es Salaam. Mjema ameamuru nyumba hizo zivunjwe kupisha mkondo huo.
 Diwani wa Kata ya Majohe, Waziri Mweneviale akimuonesha Mjema baadhi ya nyumba ambazo zimejengwa kwa kuziba mkondo wa maji eneo la Majohe, Dar es Salaam. Mjema ameamuru nyumba hizo zivunjwe kupisha mkondo huo.
 Mjema akikagua moja kati ya nyumba zilizojengwa kwenye mkondo wa maji.
 Msingi wa nyumba ukiendelea kujengwa kwenye mkondo wa maji licha ya uongozi wa
serikali ya Kata ya Majohe kuwakataza kujenga katika eneo hilo.
 Wananchi wa Gongo la Mboto wakiangalia jinsi Mto Msimbazi ulivyosababisha
maporomoko baada ya kufurika kufuatia mvua kubwa za masika zinazoendelea kunyesha sasa.
 Daraja linalounganisaha Gongo la Mboto na Ulongoni A, limezungushiwa utepe ili watu wasipite baadaya kuathiriwa na mafuriko.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala akipita kwenye mfereji wa maji alipokwenda kukagua daraja
 la Ulongoni A.

 Nyumba iliyopo kando ya mto Msimbazi Ulongoni A, ikiezuliwa mabati  baada ya kuona imo hatarini kuathiriwa na mto huo.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala akipita kwenye mfereji wa maji alipokwenda kukagua daraja  la Ulongoni A.
Mjema akisafiri kwa baada ya kumaliza kugua athari za mvua katika daraja la Ulongoni A.
KWA HISANI YA KAMANDA WA MATUKIO BLOG 0715264202

OFA OFA OFAAAAAAAAAA


RC MAKALLA ATAKA KANISA LA MORAVIAN NA WANANCHI WAKAE WAZUNGUMZE KUMALIZA MGOGORO

SERIKALI mkoani Mbeya imesema ipo haja ya pande mbili kuridhiana ili kumaliza mgogoro wa ardhi uliopo kati ya Kanisa la Moravian Tanzania na wakazi wa kijiji cha Ilolo wilayani Rungwe.

Kwa mujibu wa Mkuu wa mkoa wa Mbeya,Amos Makalla mgogoro huo uliodumu kwa zaidi ya miaka 27 bado haujamalizika kwakuwa pande hizo mbili zinaendelea kuvutana lakini amesema anaimani baada ya jitihada nyingi zinazofanyika unaweza ukamalizika iwapo pande hizo zitaridhiana.

Makalla amebainisha hayo kwenye Kikao cha kusikiliza kero za wananchi kilichofanyika wilayani Rungwe ambapo baadhi ya wakazi wa kijiji cha Ilolo walifika na kuwasilisha kero ya kulitaka kanisa kuwaachia ardhi yao.

Hata hivyo kwenye kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Rungwe,Bibi Loema Peter amesema ni vema wakazi wa kijiji hicho wakawa watulivu na kufuata maelekezo waliyopeana siku chache zilizopita ili kusaidia kumalizika kwa mgogoro.

Bi Peter amesema yapo mambo ambayo wamekubaliana yatekelezwe kila upande hatua iliyotokana na ushauri uliotolewa na kamati maalumu iliyoundwa na mkoa kufuatilia mgogoro huo.

Kwa upande wake Afisa ardhi mkoa wa Mbeya,Enock Kyando amesema mmiliki halali wa eneo linalogombaniwa ni kanisa la Moravian lakini kwakuwa uongozi wa kanisa uko radhi kutoa sehemu ya eneo lake kwa wananchi ni vema pande hizo zikakaa na kukubaliana.

Kufuatia hali hiyo,Makalla aliwataka wananchi kuwa na subira lakini akawataka pia waone uchu wa kumaliza mgogoro baina yao na kanisa ili kwa pamoja waweze kuishi kwa amani na utulivu.

Makalla ameahidi kufika kijijini Ilolo ili kutangaza maazimio yatakayokuwa yamefikiwa baada ya taratibu za pande zote zinazoshughulika na mgogoro huo kukamilika.

WAKATI HUO HUO

SERIKALI mkoani Mbeya imeagiza maafisa watendaji wa vijiji na Kata wanaoendelea kutumia majengo ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) kama Ofisi zao waondoke mara moja na kutafutiwa ofisi zao.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla alitoa agizo hilo kwenye kikao cha Kusikiliza Kero za wananchi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Ualimu Tukuyu kilichopo Msasani wilayani Rungwe na kuwakutanisha wananchi wa halmashauri za Busokelo na Rungwe.

Makalla alisema halmashauri inapaswa kuwajibika kwa kuwatafutia Maafisa watendaji Ofisi zao ili kuondoka kwenye mfumo wa chama kimoja uliokuwa ukiruhusu maafisa hao kutumia majengo ya chama kufanya shughuli zao.

Alisema kuondoka kwa maafisa hao kwenye majengo ya CCM pia kutawezesha kuondokana kwa sintofahamu za kiutendaji zinazojitokeza hususani wakati wa changuzi ambapo Ofisi hizo lazima zihudumie watu kutoka itikadi za vyama tofauti.

“Wakati wa uchaguzi mtendaji unatakiwa uhesabie kura na utangaze matokeo ofisini kwako sasa pale unapokuwa kwenye ofisi za CCM halamu unatangaza mgombea wa chama hicho hicho ndiyo ameshinda,au mgombea wa chama kingine ameshinda halafu uko ndani ya jengo la CCM lazima itakupa utata.Hii iliwezekana wakati wa mfumo wa chama kimoja lakini kwa sasa nataka Mkurugenzi maafisa hawa watafutiwe ofisi zao waondoke kwenye majengo ya chama”alisisitiza Makalla.

“Najua zipo propaganda kwa baadhi ya watu wasio na uelewa kuwa oooh endeleeni kukaa humo humo kwakuwa ofisi tulijenga wote wakati wa mfumo wa chama kimoja. Hao ni waongo hivi mnapomchangia mtu Harusi siku wakiachana mnakwenda kudai michango yenu?”alihoji.

Makalla aliyasema hayo kufuatia baadhi ya viongozi na wanachama wa CCM kuwasilisha kero kwenye kikao hicho juu ya uwepo wa Baadhi ya maafisa watendaji wanaoendelea kutumia majengo ya chama hicho kama ofisi zao na kusababisha baadhi ya shughuli za chama kukwama.