JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
Ofisi ya Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa
Mbeya,
Namba ya simu 2502572
S. L. P. 260,
Fax - +255252503734
MBEYA.
E-mail:- rpc.mbeya@tpf.go.tz
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 03.03.2018.
Jeshi
la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kukabiliana na vitendo vya uhalifu ili
kuhakikisha kuwa wageni na wakazi wa Mkoa huu wanaendelea kuwa salama na mali
zao. Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea kushirikiana na wananchi
na wadau wengine wa usalama na kufanikiwa kupata mafanikio makubwa ikiwa ni
pamoja na kukamata watuhumiwa mbalimbali wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu
@ wakorea.
KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA WANAOJIHUSISHA
NA UHALIFU @ WAKOREA.
Jeshi
la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanya Operesheni maalum pamoja na misako katika
maeneo mbalimbali ya Jiji la Mbeya. Operesheni hii ililenga kukamata wahalifu
mbalimbali likiwemo kundi la vijana wanaojiita Wakorea ambao wamekuwa wakifanya vitendo vya uhalifu na kuhatarisha
usalama wa raia na mali zao.
Operesheni
hii imefanyika katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Mbeya ambayo ni Ivumwe,
Mwakibete, Mwambene, Mama John, Ilomba, Mafiati, Makunguru, Iyela na Isyesye.
Katika
Operesheni hii maalum, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa
sita [06] kutokana na tuhuma za
kujihusisha na vitendo vya kiuhalifu. Watuhumiwa hao wamefahamika kwa majina
ya:-
1.
KELVIN RAPHAEL
[22] Mwakibete Bomba mbili ambaye ndiye kiongozi wa kundi hili la uhalifu @
Wakorea.
2.
CLEMENCE CHRISTOPHER @ MWAKALINGA [23] Mkazi wa Mwakibete Viwandani.
3.
CHARLES MWASUMBI [21] Mkazi wa Mwakibete
4.
EDGA EDWARD
[20] Makondeko Mwakibete
5.
IPYANS NDUNGURU
[21] Mkazi wa Mwakibete
6.
ADEN MWALUKASA
[35] Mkazi wa Mwakibete
Pia
katika Operesheni hii maalum ya kuwasaka vijana wanaojihusisha na uhalifu hapa
Jijini Mbeya, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia vijana watatu [03] kutokana na tuhuma za kujihusisha na vitendo vya uvunjaji nyakati
za usiku na mchana. Watuhumiwa hao wamefahamika kwa majina ya:-
1.
GODFREY JOSEPH @ MHENGA [20] Mkazi wa Ilemi Mapelele
2.
GODFREY PAUL @ MWAKASAJE [39] Mkazi wa Ilemi Mapelele
3.
MTEMI YAHAYA @ MWASANGA [42] Mkazi wa Uyole
Watuhumiwa
hao baada ya kukamatwa na kupekuliwa walikutwa na vifaa mbalimbali walivyokuwa
wakivitumia kuvunjia ambavyo ni:-
1.
Bisibisi – 03
2.
Nyundo – 01
3.
Mkasi – 01
Aidha
watuhumiwa hao walikutwa na mali mbalimbali za wizi:-
1. Flat Screen aina ya Home base
2. Flat Screen aina ya Samsung
3. TV ya kawaida aina ya Home base
4. Sub Woofer 01
5. Deck 03 aina ya Singsung 02 na Fusion 01.
Aidha
mwanzoni mwa mwezi Januari, 2018, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilifanikiwa
kuwakamata watuhumiwa nane [08]
kutokana na kujihusisha na vitendo vya uhalifu katika maeneo mbalimbali ya Jiji
la Mbeya ambao walifikishwa Mahakamani na kwa sasa wanatumikia vifungo vya nje.
Pia
watuhumiwa kumi na mbili [12] ambao
walikamatwa hivi karibuni katika Operesheni/Misako iliyofanyika huko katika
maeneo ya Ilemi, Juhudi, Makunguru na Mwenge hapa Jijini Mbeya ambao kesi zao
zinaendelea katika Mahakama ya Mwanzo Iyunga
Watuhumiwa
wengine watafikishwa Mahakamani mara tu baada ya Upelelezi kukamilika.
WITO:
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi MOHAMMED R. MPINGA anatoa wito kwa vijana na jamii kwa ujumla
kuacha kujihusisha na vitendo vya uhalifu kwani ni kinyume cha sheria na badala
yake wajishughulishe na kazi halali kwa ajili ya kujipati kipato. Aidha anatoa
onyo kali wafanyabiashara ya vilezi kufuata sheria na taratibu za biashara yao
ikiwa ni pamoja na kufungua na kufunga sehemu zao za biashara muda sahihi kwa
mujibu wa sheria.
Imesainiwa na:
[MOHAMMED R. MPINGA - DCP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA