Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, June 14, 2023

SINGIDA BIG STARS YAPIGWA MNADA

Na Lyamba Lya Mfipa
Uongozi wa klabu ya Singida Big Stars umefikia makubaliano ya kuiuza timu hiyo kwa wamiliki wa Fountain Gate.

Mtendaji Mkuu wa Singida Big Stars John Kadutu amesema hayo mkoani Dar es Salaam katika mkutano wake na waandishi wa habari.
Amesema wameridhia kuiuza timu hiyo kwa fountain Gate, lakini kwa sharti la timu hiyo kubakia mkoani Singida.
Kwa upande wake Mmiliki mpya wa Timu hiyo Japhet Makau amesema, fursa hiyo imekuja katika wakati muafaka ndio maana wamemua kuichangamkia.
Kwa sasa jina la Singida Big Stars limebadilishwa na kuitwa Singida Fountain Gate Football Club.

No comments:

Post a Comment