Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, April 29, 2012

CHUTCU WAFANYA MKUTANO WA 12

 Katibu tawala mkoa wa Mbeya akisoma hotuba ya mkuu wa mkoa huo Abbas Kandoro alipomwakilisha kufungua mkutano wa 12 wa chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Tumbaku wilayani Chunya(CHUTCU)
 

WAKULIMA wa zao la tumbaku wamehimizwa kuanza kujikita katika kilimo
cha mazao mbadala kutokana na zao hilo kuendelea kupigwa vita na
wanaharakati mbalimbali duniani.

Katibu tawala mkoa wa Mbeya Marium Mtunguja amesisitiza hayo kwenye
mkutano wa 12 wa chama kikuu cha ushirika wa wakulima wa tumbaku
wilayani Chunya(CHUTCU).

Mtunguja alisema kauli hiyo hailengi kukataza kilimo cha zao hilo bali
kuanza kuchukua tahadhari kwakuwa hakuna ajuaye nini yatakuwa matokeo
ya hoja zinazojadiliwa na kupiganiwa na wanaharakati wanaopinga
uvutaji wa sigara.

Aliyataja mazao yanayoweza kupewa nafasi na kuleta manufaa makubwa kwa
wakulima kuwa ni pamoja na ufuta unaostawi katika ardhi ya wilaya ya
Chunya,ufuta na alizeti.

Alisisitiza pia CHUTCU kuona uwezekano wa kuanzia chama cha kuweka na
kukopa (Saccos) ili kuwawezesha wanachama kuachana na mikopo iliyo na
riba kubwa kutoaka katika taasisi kubwa za kifedha.

Katibu tawala huyo aliwataka wanaushirika kuhakikisha wanaviimarisha
vyama vyao ili visishuke na kufa kama ilivyotokea kipindi cha miaka ya
nyuma badala yake wajiwekee mikakati ya kuviendelea na kuwa na nguvu
zaidi.

“Tuwe tunajiuliza ilikuwaje vyama vya ushirika vikafa.Sababu zipi.Ni
kutokana na uongozi mbovu uliojikita katika kuchukua mikopo mikubwa na
kuitumia vibaya kinyume na utaratibu sahihi.Sasa tusikubali kurudi
huko.Sasa tusonge mbele”.

Alibainisha kuwa kuendelezwa kwa vyama hivyo kutakuwa chachu ya
mafaniko kwa mtu mmoja mmoja na pia wilaya kwa kukuza uchumi
utakaowezesha kufanikishwa kwa shughuli mbalimbali za kimaendeleo hasa
elimu na makazi bora.


Kwa upande wake mwenyekiti wa CHUTCU Sebastian Mogela alikiri ushirika
kuendelea kuyategemea makampuni ni kuchelewa kupiga hatua kimaendeleo
akisema yapo kwaajili ya kufanya biashara yapate faida na si kutoa
misaada kwa wakulima.

Mogela alisisitiza umuhimu wa chama kikuu hicho kuwa na maofisa ugani
wake ili waweze kusimamia kwa karibu kilimo hicho na kuleta manufaa
zaidi kwa wakulima badala ya kuendelea kutumia wataalamu wa makampuni
yanayonunua tumbaku.

“Haiwezekani tukajitegemea kwa pembejeo pekee wakati wataalamu
wanaosimamia matumizi ya pembejeo hizo wanatoka kwingine.Lazima
usimamizi wake utalenga kuinufaisha kampuni yake na wala siyo sisi”.

MBEYA WALIVYOSHEREHEKEA MIAKA 48 YA MUUNGANO WA TANZANYIKA NA ZANZIBAR KATIKA KIJIJI CHA CHALANGWA WILAYANI CHUNYA

 Baadhi ya wakuku wa wilaya za mkoani Mbeya waliohudhuria sherehe za muungano katika kijiji cha Chalangwa wiolayani Chunya wakifuatialia kwa makini hotuba ya kaimu mkuu wa mkoa Evance Balama ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Mbeya.
 Wananchi waliohudhuria sherehe za miaka 48 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Mmoja wa wanafunzi wa shule ya sekondari Chalangwa akijimwaga mbele ya watazamaji wakati wa ngonjera iliyoandaliwa na wanafunzi hao
Mambo ya KIDUKU hayakuachwa nyuma,Huyu ndo bingwa wa viduku kwa shule nzima ya sekondari Chalangwa
Mikogo,na jinsi alivyokuwa akimwaga tungo zake ilikuwa burudani kwa kila aliyefika uwanjani hapa
Wapiga ngoma nao walikuwa na mambo yao yaliyonogesha zaidi sherehe hizi 
Chifu wa kabila la Wasafwa akiimba shairi aliloliandaa kwaajili ya muungano
 Baadhi ya wananchi walishindwa kuficha hisia zao na kuamua kuingia uwanjani kuonesha makeke wakati bendi ya muziki wa asili wa kabila la wasafwa ikitumbuiza
Inaonesha utamu ulikolea mpaka mwananchi huyu akaamua atumie viungo vyake vyote kucheza muziki wa Kisafwa.

Thursday, April 26, 2012

Wednesday, April 25, 2012

WAUZAJI,WANUNUZI KAHAWA MBICHI KUKIONA CHA MOTO


SERIKALI wilayani Mbozi imesema itawachukulia hatua za kisheria watu wote watakaohusika na biashara ya kahawa mbichi katika msimu ujao wa mavuno ya zao hilo.

Mkuu wa wilaya hiyo Gabriel Kimolo ametoa onyo hilo leo alipotoa salamu za serikali katika kikao cha kawaida cha baraza la madiwani.

Kimolo amesema licha ya serikali kupitia wizara husika kutoa maamuzi yaliyotokana na ushauri wa vikao halali vya serikali ya wilaya na mkoa kukataza ununuzi huo bado kuna watu wana dhamira ya kukiuka agizo.

Amesema watu hao wanajaribu hata kughushi barua na kuzituma kwa utawala wa wilaya na mkoa kuarifu kuwa ununuzi wa kahawa mbichi umeruhusiwa na ofisi ya waziri mkuu jambo ambalo halina ukweli.

Amesisitiza kuwa mkono wa sheria katika uwajibishaji utawalenga wauzaji na pia wanunuzi wa kahawa mbichi kwakuwa wote watakuwa wanakiuka agizo hilo.

Monday, April 23, 2012

WATOTO WAOKOTA BEGI LENYE MAITI

WATOTO watano waliokuwa wakioga katika mfereji wa Mwanjejele, uliopo Igurusi Wilaya ya Mbarali, Aprili 22 mwaka huu majira ya saa tisa alasiriwaliokota begi lililokuwa linaelea katika maji ya mfereji huo na kukuta maiti ya mtoto mchanga.

Maiti hiyo ikiwa imeharibika vibaya kutokana na kuoza ndipo walipolichukua begi hilo na kulipeleka katika Kituo cha Polisi cha Igurusi.
Mmoja wa majeruhi wa  kati ya 40 walionusurika kifo baada ya basi waliokuwa wakisafiri aina ya Coaster, lenye nambari za usajili T 374 AVR, kupinduka lilipogongwa kwa nyuma na basi jingine la kampuni ya El Saedy lenye nambari T 499 AVG. Tukio lililotokea Aprili 23 mwaka huu saa moja asubuhi eneo la Imezu na Inyala Wilaya ya Mbeya Vijijini.
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Imezu wakikwa katika Hospitali ya Rufaa, wakisubiri kupatiwa matibabu, mara baada ya basi aina ya Coaster waliyokuwa wakisafirikia  enye nambari za usajili T 374 AVR, kupinduka lilipogongwa kwa nyuma na basi jingine la kampuni ya El Saedy lenye nambari T 499 AVG. Tukio lililotokea Aprili 23 mwaka huu saa moja asubuhi eneo la Imezu na Inyala Wilaya ya Mbeya Vijijini.
  Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Imezu wakikwa katika Hospitali ya Rufaa, wakisubiri kupatiwa matibabu, mara baada ya basi aina ya Coaster waliyokuwa wakisafirikia  enye nambari za usajili T 374 AVR, kupinduka lilipogongwa kwa nyuma na basi jingine la kampuni ya El Saedy lenye nambari T 499 AVG. Tukio lililotokea Aprili 23 mwaka huu saa moja asubuhi eneo la Imezu na Inyala Wilaya ya Mbeya Vijijini.
Basi aina ya Coaster waliokuwa wakisafiria abiria zaidi ya 40, lenye nambari za usajili T 374 AVR, likiwa limepinduka baada ya kugongwa kwa nyuma na basi jingine la kampuni ya El Saedy lenye nambari T 499 AVG. Tukio lililotokea Aprili 23 mwaka huu saa moja asubuhi eneo la Imezu na Inyala Wilaya ya Mbeya Vijijini.
 Basi aina ya Coaster waliokuwa wakisafiria abiria zaidi ya 40, lenye nambari za usajili T 374 AVR, likiwa limepinduka baada ya kugongwa kwa nyuma na basi jingine la kampuni ya El Saedy lenye nambari T 499 AVG.
Basi la kampuni ya El Saedy lenye nambari T 499 AVG lililohusika katika ajali, baada ya kuligonga kwa nyuma basi aina ya Coaster enye nambari za usajili T 374 AVR ambapo zaidi ya abiria 40 kunusurika kifo. Tukio lililotokea Aprili 23 mwaka huu saa moja asubuhi eneo la Imezu na Inyala Wilaya ya Mbeya Vijijini.(Picha na Ezekiel Kamanga, Mbeya.)

MKUTANO MKUU WA MWAKA 2012 WA TFF


RAIS WA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA, LEODGAR CHILLA TENGA

MKUTANO MKUU WA MWAKA 2012 WA TFF
Mkutano Mkuu wa Mwaka (AGM) wa 2012 wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) umefanyika kwa siku mbili (Aprili 21-22 mwaka huu) kwenye ukumbi wa NSSF Waterfront na kuhudhuriwa na wajumbe 104. Mkutano ulipokea taarifa, kufanya uamuzi katika masuala mbalimbali na mengine yaliyojitokeza kama ifuatavyo;

EL MAAMRY, NDOLANGA WATUNUKIWA URAIS WA HESHIMA
AGM ilipitisha pendekezo la kuwatunuku urais wa heshima wa TFF, Alhaji Said Hamad El Maamry na Muhidin Ahamadi Ndolanga lililowasilishwa na Mwenyekiti wa mkutano huo ambaye pia ni Rais wa TFF, Leodegar Tenga.

Alhaji El Maamry ambaye ni mjumbe wa heshima wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) alikuwa Mwenyekiti wa TFF wakati huo ikiitwa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) kuanzia mwaka 1973 hadi 1986. Alhaji Ndolanga aliongoza FAT kuanzia mwaka 1993 hadi 2004.

BAJETI YA MWAKA 2012
Bajeti ya Mwaka 2012 ya sh. 7,246,628,650 kwa ajili ya matumizi ya TFF ilipitishwa. Kwa mwaka 2012 TFF inatarajia kukusanya sh. 7,572,991,433 kupitia vyanzo mbalimbali.

Vyanzo hivyo ni viingilio vya uwanjani vinavyotarajiwa kuingiza asilimia 22 ya mapato yote, udhamini (asilimia 74) na vyanzo vingine kama haki za matangazo ya televisheni, ada za ushiriki wa timu katika mashindano mbalimbali, misaada kutoka FIFA na CAF ambayo kwa pamoja vinatarajiwa kuingiza asilimia nne ya mapato yote.

KAMATI YA LIGI YA TFF
Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) itaendelea na mchakato wa kupendekeza mifumo mitatu tofauti ya chombo kitakachosimamia/kuendesha Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ikieleza faida na athari za kila mfumo uliopendekezwa na baadaye kuwafanya mawasilisho (presentation) kwenye Kamati ya Utendaji.

Baada ya kuwasilisha mifumo hiyo kwa Kamati ya Utendaji, Kamati ya Ligi itapendekeza mfumo upi kati yao hiyo inaoona unafaa kabla ya kufanyika uamuzi wa mwisho.

Lengo la kuunda chombo maalumu cha kuendesha ligi ni kuongeza ufanishi katika uendeshaji wa VPL na FDL, na pia kuifanya Sekretarieti ya TFF kushughulikia zaidi shughuli za maendeleo.

UUZWAJI WA TIMU
Uuzaji wa timu linabaki kuwa suala la kisheria. Lakini TFF imeweka utaratibu ufuatao; lazima Mkutano Mkuu wa klabu husika uidhinishe uuzaji, na timu ikishauzwa inabaki katika mkoa husika.

MFUMO WA MASHINDANO
Kwa vile kuna tatizo la ligi mbalimbali kuwa fupi, hali inayosababisha baadhi ya wachezaji katika madaraja ya chini kucheza ligi zaidi ya moja katika msimu mmoja, mfumo wa ligi/mashindano utaangaliwa upya.

Mfumo uliopo sasa uliwekwa kwa ajili ya kuvutia uwekezaji katika mpira wa miguu ambapo mwekezaji anaweza kuanzisha timu, na ndani ya miaka mitatu ikacheza Ligi Kuu. Pili, ilikuwa ni kuondoa mlolongo mrefu wa ligi, na kuwafanya wanachama wa TFF (mikoa) nao kuendesha ligi zao mikoani.

Ijulikane kuwa ligi za mikoa (regional leagues) zinachezwa. Kwa sababu TFF inaendeshwa kwa mfumo wa shirikisho (federation), nia ni wanachama wa federation nao kuwa na majukumu ya kusimamia na kuendesha ligi, kwa vile TFF haiwezi kusimamia ligi zote.

MAREKEBISHO YA KATIBA
Mkutano Mkuu wa TFF umepitisha marekebisho ya Katiba katika maeneo mawili; moja ni kuanzisha Baraza la Wadhamini ambalo linatakiwa kuwa na wajumbe wasiopungua watatu na wasiozidi watano.

Marekebisho mengine ni kuongeza idadi ya kanda kutoka kumi na moja za sasa hadi 13. Marekebisho hayo yamefanyika kutokana na Serikali kuongeza mikoa mipya ya kijiografia.

Kanda mpya sasa zitakuwa Kagera/Geita, Arusha/Manyara, Kilimanjaro/Tanga, Katavi/Rukwa, Njombe/Ruvuma, Dodoma/Singida, Dar es Salaam, Shinyanga/Simiyu, Mwanza/Mara, Lindi/Mtwara, Kigoma/Tabora, Mbeya/Iringa na Pwani/Morogoro.

Ukiondoa mamlaka ya uteuzi aliyonayo Rais kwa mujibu wa Katiba ya TFF, wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji huchaguliwa kwa kanda.

HESABU ZILIZOKAGULIWA
Mkutano Mkuu ulipitisha hesabu zilizokaguliwa za mwaka 2010 (Audited Accounts) , na pia kuiteua kampuni ya ukaguzi wa hesabu ya TAC Associates kuwa mkaguzi wa hesabu za TFF kwa kipindi cha miaka minne ijayo.

YANGA YAOMBA RADHI MKUTANO MKUU
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga ambaye pia mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF akiwakilisha klabu za Mkoa wa Dar es Salaam, Mohamed Bhinda aliwaomba radhi wajumbe wa Mkutano Mkuu kwa kitendo cha wachezaji wake kumpiga mwamuzi Israel Nkongo kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya Azam iliyochezwa Machi 10 mwaka huu.

Pia alimuomba Rais wa TFF, Leodegar Tenga kutoa msamaha wa adhabu ya kulipa faini iliyotolewa na Kamati ya Ligi ya TFF kwa wachezaji wawili wa Yanga ambao mpaka sasa hawajalipa faini hiyo.

Rais Tenga alimshukuru Bhinda kwa ujasiri alioonesha wa kuomba radhi mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF kwa kitendo kile. Aliongeza kuwa kwa vile yeye ni muumini wa kanuni, na adhabu hizo zimetolewa kwa mujibu wa kanuni hawezi kutoa msamaha, hivyo wachezaji hao walipe faini hizo.

Pia Rais Tenga alisema binafsi haziingilia kamati za TFF katika uamuzi ambao zinafanya kwa vile zina watu waadilifu, na angekuwa yeye binafsi ndiye anayetoa adhabu, angetoa adhabu kali zaidi kwa vile vitendo vya kupiga waamuzi havikubaliki katika mchezo wa mpira wa miguu.

KANUNI ZA NIDHAMU, MAHAKAMA YA USULUHISHI
Akizungumza wakati wa kufunga mkutano huo, Rais Tenga aliwaambia wajumbe kuwa Kanuni za Nidhamu (Disciplinary Code) za TFF na uundaji wa Mahakama ya Usuluhishi (Arbitration Tribunal) ya TFF ambacho ndicho kitakuwa chombo cha juu cha kutoa haki kwa masuala ya mpira wa miguu nchini vitakamilika mwaka huu.

Pia TFF itaendelea kutafuta wadhamini kwa ajili ya timu za Taifa za vijana na wanawake, itaendelea kuendesha semina na makongamano katika nyanja mbalimbali za mpira wa miguu, kutengeneza mtaala wa academy na kutengeneza mpango wa maendeleo (Comprehensive Plan) baada ya ule wa awali kumalizika mwaka huu.

KIMONDO KILICHOPO WILAYANI MBOZI

Hii ni picha ya kimondo kilichopo wilayani Mbozi mkoani Mbeya.Ni fursa ya kipekee ya kitalii ambayo mkoa haujaitumia ipasavyo kwa kuitangaza ipasavyo duniani

MADEREVA ARUSHA-MBEYA WATUHUMIWA KUSAFIRISHA MIRUNGI

Madereva wa mabasi yanayosafirisha abiria kwa safari za Arusha Mbeya wanatajwa kuwa miongoni mwa wasafirishaji wakubwa wa Mirungi kutoka jijini Arusha kupeleka mikoa ya Dodoma,Iringa na Mbeya.

Uchunguzi uliofanywa na Lyamba Lya Mfipa umebaini kuwa hata pale askari wa barabarani (Traffic) wanapokuwa wamepewa taarifa juu ya dereva kupakia milungi katika gari yake na kupewa namba za basi husika wamekuwa wakishindwa kuwa kamata kwakuwa madereva hao hubadikli vibao vinavyoelekeza safari za gari husika kila wanapokaribia kituo cha askari hao

LULU MAHAKAMANI TENA

Mapema leo: Picha za Lulu Alipo pelekwa Kizimbani kwa Ulinzi mkali .. Baba mzazi alikuwepo pia mahakamani hapo

Elizabeth Michael 'Lulu' akiwa chini ya ulinzi mkali.
Lulu akiwa kawekwa mtu kati.…
Elizabeth Michael 'Lulu' akiwa chini ya ulinzi mkali.
Lulu akiwa kawekwa mtu kati.

Askari wakidumisha ulinzi nje ya mahakama.

...Askari huyu akiandaa njia kabla ya Lulu kupitishwa.
Karandinga lililomleta Lulu mahakamani leo.
Baba mzazi wa Lulu nae alikuwepo mahakamani hapo.
Mwigizaji Maarufu wa filamu za Kibongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ leo majira ya saa nne asubuhi amepandishwa kizimbani kwa mara ya pili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa shitaka la kumuua Steven Kanumba. Baada ya kusomewa shitaka hilo na Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Mahakama hiyo Elizabeth Kaganda mbele ya Hakimu Rita Tarimo hakutakiwa kujibu lolote. Mwendesha Mashitaka huyo alisema upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamailika hivyo kesi hiyo iliahirishwa mpaka Mei 7 mwaka huu.
PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS/GPL
Sindano ya ganzi yamsababishia mauti mtoto Tumaini Rataniel Mtajiha (5), mkazi wa Kijiji cha Hagomba Kata ya Itaka baada ya kuchomwa na daktari wa zahanati binafsi ya Sisika, inayomilikiwa na mwalimu mmoja katika Mtaa wa Ichenjezya, Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea Aprili 22 mwaka huu majira ya saa tano asubuhi baada ya mtoto huyo kufikishwa katika Zahanati binafsi, akiwa na jipu katika makalio ndipo Daktari alipompokea na kumtoza shilingi 20,000 baba mzazi wa marehemu Bwana Rataniel Mtajiha (45), ili apewe huduma.
Sababu ya kuchomwa sindano ya ganzi ni kutokana na mtoto huyo kuonaonekana ni mwoga hivyo achomwe sindano hiyo, na baada ya kuchomwa mtoto huyo alifariki papo hapo.
Baada ya tukio hilo Bwana Mtajiha alitoa taarifa Kituo cha Polisi Vwawa, ambapo walifika na kumchukua Daktari huyo (Jina linahifadhiwa), mwili wa mtoto na jalada lake pamoja na  sampuli ya dawa alizotumia hadi kwenye Hospitali ya Wilaya ili kufanyiwa uchunguzi majira ya saa 10:00 jioni.
Aidha, baada ya kutafakari kwa kina Hospitali hiyo ya wilaya, walitoa taarifa mkoani na kuagiza mwili ufanyiwe uchunguzi Aprili 23 mwaka huu, baada ya jopo la mkoani kuwasili wilayani Mbozi ili kufanya uchunguzi wa kina.
Kaimu kamanda wa Polisi mkoani Mbeya hakuweza kupatikana kuthibitisha tukio hili, na hivi sasa Daktari wa Zahanati hiyo anashikiliwa na Kituo cha polisi Vwawa akisubiri uchunguzi kufanyika.
Wakati huo huo baba mzazi Bwana Mtajiha, amesema hakutegemea mwanae kufikwa na mauti kwani, muda wote alikuwa anacheza licha  ya kukabiliwa na jipu hilo. 
 
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.