Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, April 21, 2012

SHIRIKISHO la vyama huru vya wafanyakazi nchini (TUCTA) limesema linaandaa utaratibu wa kuwaweza wafanyakazi kukutana na kubadilishana uzoefu kupitia makongamano yatakayokuwa yanafanyika katika kanda mbalimbali
Mwenyekiti wa TUCTA taifa Omary Ayub Juma ameyasema hayo jijini Mbeya wakati akifunga mafunzo ya siku tano ya wafanyakazi kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania bara yaliyokuwa yakiendeshwa katika chuo cha wafanyakazi kilichopo jijini hapo.
Juma amesema kupitia makongamano hayo licha ya wafanyakazi kujadili namna ya kukabililiana na changamoto mahala paa kazi pia wataweza kujikumbusha wajibu wao hasa kwa kujifunza zaidi juu ya sheria za kazi.

Aidha mwenyekiti huyo pia amesema TUCTA inaangalia uwezekano wa kukiboresha chuo cha wafanyakazi Mbeya kutokana na madhari yake kutoendana na hadhi yake.

Ameyasema hayo kufuatia wahitimu wa mafunzo hayo kupitia risala iliyosomwa na mwenzao Sima Kazaula kuelezea kutoridhishwa na hali ya majengo ya chuo wakisema yamechakaa na yanahitaji maaboresho makubwa.

No comments:

Post a Comment