WAJASIRIAMALI WAPEWA MAFUNZO
WASHINDI 12 wa shindano la Safari Wezesha
linaloendeshwa na Kampuni ya Bia nchini (TBL) kutoka mikoa ya nyanda za juu
kusini wamepewa mafunzo ya ujasiliamali kabla ya kukabidhiwa vifaa vya
kuwasaidia kuendeleza biashara zao kwa ufanisi.
Wakufunzi kutoka kampuni ya TIP ya Dar
es Salaam ndiyo waliopewa dhamana ya kuendesha mafunzo hayo yaliyodumu kwa muda
wa siku tano jijini Mbeya.
Mratibu wa mafunzo kutoka kampuni ya
TBL, Onesmo Swila amesema washindi hao wanatarajiwa kuwezeshwa kwa kukabidhiwa
vifaa hivyo Mei 26, mwaka huu.
Swila alifafanua kuwa jumla ya
wajasiriamali 263 walijitokeza kushiriki shindano hilo kwa kujaza fomu za
ushiriki kutoka mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Amesema baada ya fomu hizo kupitiwa,
wajasiriamali 20 ndio waliokidhi vigezo vya kupewa msaada wa Safari Wezesha kwa
ajili ya kusaidiwa kuendeleza biashara zao.
Mwenyekiti wa wajasiriamali hao katika
mafunzo yao, Festo Sikagonamo amesema mafunzo hayo yaliyoanza tangu Aprili 16,
mwaka huu yamewapa ujuzi na maarifa ya kuziinua biashara zao hata kabla ya
kukabidhiwa vifaa vya Safari Wezesha.
No comments:
Post a Comment