Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, April 23, 2012

LULU MAHAKAMANI TENA

Mapema leo: Picha za Lulu Alipo pelekwa Kizimbani kwa Ulinzi mkali .. Baba mzazi alikuwepo pia mahakamani hapo

Elizabeth Michael 'Lulu' akiwa chini ya ulinzi mkali.
Lulu akiwa kawekwa mtu kati.…
Elizabeth Michael 'Lulu' akiwa chini ya ulinzi mkali.
Lulu akiwa kawekwa mtu kati.

Askari wakidumisha ulinzi nje ya mahakama.

...Askari huyu akiandaa njia kabla ya Lulu kupitishwa.
Karandinga lililomleta Lulu mahakamani leo.
Baba mzazi wa Lulu nae alikuwepo mahakamani hapo.
Mwigizaji Maarufu wa filamu za Kibongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ leo majira ya saa nne asubuhi amepandishwa kizimbani kwa mara ya pili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa shitaka la kumuua Steven Kanumba. Baada ya kusomewa shitaka hilo na Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Mahakama hiyo Elizabeth Kaganda mbele ya Hakimu Rita Tarimo hakutakiwa kujibu lolote. Mwendesha Mashitaka huyo alisema upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamailika hivyo kesi hiyo iliahirishwa mpaka Mei 7 mwaka huu.
PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS/GPL

No comments:

Post a Comment