Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, April 21, 2012

WAZIRI KABAKA ALIPOWAFUNDA WAFANYAKAZI NSSF

VIONGOZI na wajumbe wapya wa Baraza kuu la wafanyakazi wa shirika la hifadhi ya jamii (NSSF) wametakiwa  kufanya kazi kwa uadirifu wakitambua fika kuwa nyuma yao wapo wafanyakazi wanaowategemea kuleta ufanisi kiutendaji.
 Waziri wa Kazi na Ajira Gaudencia Kabaka amesisitiza hayo (April 18) wakati akifungua mkutano wa 38 wa baraza kuu la wafanyakazi wa NSSF uliofanyika jijini Mbeya na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali kutoka ofisi za matawi yote ya shirika hilo.
Waziri Kabaka pia amesisitiza shirika hilo kuona umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika mikoa mbalimbali iliyo na fursa za uwekezaji ikiwemo mkoa wa Mbeya hasa katika mradi wa Makaa ya mawe wa Kiwira mara tu serikali itakapotoa maamuzi.
 
Awali mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro ameelezea kutoridhika na uwekezaji wa miradi ya kimaendeleo unaofanywa na NSSF akisema mkoani Mbeya akisema bado haukidhi ikilinganishwa na ilivyofanya kwa mikoa mingine.
Kandoro amesema upo umuhimu mkubwa wa viongozi wa shirika hilo kufanya mazungumzo na uongozi wa halmashauri ya jiji la Mbeya ili kufikia makubaliano ya kuweikeza katika miradi ya ujenzi wa masoko ya kisasa pamoja na nyumba kwaajili ya makazi hasa ikizingatiwa kuwa jiji hilo linakuwa kwa kasi ya asilimia 7.

No comments:

Post a Comment