Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, April 25, 2012

WAUZAJI,WANUNUZI KAHAWA MBICHI KUKIONA CHA MOTO


SERIKALI wilayani Mbozi imesema itawachukulia hatua za kisheria watu wote watakaohusika na biashara ya kahawa mbichi katika msimu ujao wa mavuno ya zao hilo.

Mkuu wa wilaya hiyo Gabriel Kimolo ametoa onyo hilo leo alipotoa salamu za serikali katika kikao cha kawaida cha baraza la madiwani.

Kimolo amesema licha ya serikali kupitia wizara husika kutoa maamuzi yaliyotokana na ushauri wa vikao halali vya serikali ya wilaya na mkoa kukataza ununuzi huo bado kuna watu wana dhamira ya kukiuka agizo.

Amesema watu hao wanajaribu hata kughushi barua na kuzituma kwa utawala wa wilaya na mkoa kuarifu kuwa ununuzi wa kahawa mbichi umeruhusiwa na ofisi ya waziri mkuu jambo ambalo halina ukweli.

Amesisitiza kuwa mkono wa sheria katika uwajibishaji utawalenga wauzaji na pia wanunuzi wa kahawa mbichi kwakuwa wote watakuwa wanakiuka agizo hilo.

No comments:

Post a Comment