Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, January 8, 2016

KIWANDA CHA KUTENGENEZA SABUNI CHA HI SOAP MBEYA SASA CHAANZA KULIMA BANGI

Sehemu ya mimea ya bangi ikiwa imepandwa pamoja na maharage ndani ya eneo la kiwanda cha sabuni cha Hi Soap jijini Mbeya kama ilivyokutwa na wanachama wa Chama cha waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji Tanzania(TAJATI).Kiwanda hiki kimetelekezwa kwa zaidi ya miaka 10 sasa na haijulikani mwekezaji yupi alibinafsishiwa

Sunday, January 3, 2016

FISTULA BADO NI TATIZO MBEYA!

HAMASA ndogo juu ya matibabu ya Ugonjwa wa Fistula imetajwa kuwa chanzo cha jamii inayosumbuliwa na ugonjwa huo kutojitokeza ili kupata matibabu.

Kaimu mkuu wa Kitengo cha wazazi cha Meta katika Hospitali ya Rufaa kanda ya Mbeya Dk.Godlove Mbwanji amebainisha hayo alipozungumza na waandishi wa habari juu ya mweneno wa utoaji huduma kwa wagongwa wa Fistula.

Dk.Mbwanji amesema uchunguzi unaonesha kuwa katika kipindi inapofanyika kampeni kubwa za matibabu ya ugonjwa wa Fistula ambao kimsingi hutolewa bure ndipo wagonjwa wengi hujitokeza kutibiwa na mara kampeni zinapokoma wagonjwa hujitokeza kwa kusuasua.

Amesema mwendo huo unatoa majibu yenye uhalisia kuwa wanawake wanaosumbuliwa na Fistula ni wengi miongoni mwa jamii lakini hawafiki kupata matibabu kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha juu ya ugonjwa huo.

Asema katika jamii bado kuna watu wanaojua ugonjwa huo hauna tiba,wengine hujua tiba hutolewa kwa malipo na hivyo wanaogopa gharama huku wengine pia wakiuhusisha ugonjwa huo na imani za kishirikina.

Amesema ni vema kampeni za kuwaongezea uelewa wananchi katika maeneo mbalimbali juu ya ugonjwa wa Fistula zikawa endelevu ili kuwezesha jamii kutambua kuwa ni ugonjwa unaotibiwa bure na hata wagonjwa wanaofika hurejeshewa nauli waliyojia kwa hisani ya shirika la kimataifa llinalojisgughulishaa na masuala ya Afya ya uzazi la Amref.


Aidha,Dk.Mbwanji ameyataja maeneo ya pembezoni kuwa yenye kusumbuliwa kwa kiasi kikubwa na Fistula huku Kwa mkoani Mbeya akizitaja wilaya za Mbozi,Momba na Chunya kuwa zilizo na wagonjwa wanaojitokeza kwa wingi kutibiwa ugonjwa huo.

Friday, January 1, 2016

TANZIA TANZIA TANZIA



Mhariri mkuu wa Blogu ya Lyamba Lya Mfipa Bwana Joachim Nyambo,anasikitika kutangaza kifo cha mjomba yake Nickas Nkana kilichotokea usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Tumbi iliyopo mkoani Pwani.Safari ya kusafirisha mwili wa marehemu kuelekea Sumbawanga mkoani Rukwa inatarajiwa kuanza wakati wowote mara baada ya taratibu za usafiri kukamilika.
Habari ziwafikie,ndugu,jamaa na marafiki wote.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa,jina la bwana na libarikiwe!