Mhariri mkuu wa Blogu ya Lyamba Lya Mfipa Bwana
Joachim Nyambo,anasikitika kutangaza kifo cha mjomba yake Nickas Nkana
kilichotokea usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Tumbi iliyopo mkoani
Pwani.Safari ya kusafirisha mwili wa marehemu kuelekea Sumbawanga mkoani Rukwa
inatarajiwa kuanza wakati wowote mara baada ya taratibu za usafiri kukamilika.
Habari ziwafikie,ndugu,jamaa na marafiki wote.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa,jina la bwana na
libarikiwe!
No comments:
Post a Comment