Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, January 3, 2016

FISTULA BADO NI TATIZO MBEYA!

HAMASA ndogo juu ya matibabu ya Ugonjwa wa Fistula imetajwa kuwa chanzo cha jamii inayosumbuliwa na ugonjwa huo kutojitokeza ili kupata matibabu.

Kaimu mkuu wa Kitengo cha wazazi cha Meta katika Hospitali ya Rufaa kanda ya Mbeya Dk.Godlove Mbwanji amebainisha hayo alipozungumza na waandishi wa habari juu ya mweneno wa utoaji huduma kwa wagongwa wa Fistula.

Dk.Mbwanji amesema uchunguzi unaonesha kuwa katika kipindi inapofanyika kampeni kubwa za matibabu ya ugonjwa wa Fistula ambao kimsingi hutolewa bure ndipo wagonjwa wengi hujitokeza kutibiwa na mara kampeni zinapokoma wagonjwa hujitokeza kwa kusuasua.

Amesema mwendo huo unatoa majibu yenye uhalisia kuwa wanawake wanaosumbuliwa na Fistula ni wengi miongoni mwa jamii lakini hawafiki kupata matibabu kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha juu ya ugonjwa huo.

Asema katika jamii bado kuna watu wanaojua ugonjwa huo hauna tiba,wengine hujua tiba hutolewa kwa malipo na hivyo wanaogopa gharama huku wengine pia wakiuhusisha ugonjwa huo na imani za kishirikina.

Amesema ni vema kampeni za kuwaongezea uelewa wananchi katika maeneo mbalimbali juu ya ugonjwa wa Fistula zikawa endelevu ili kuwezesha jamii kutambua kuwa ni ugonjwa unaotibiwa bure na hata wagonjwa wanaofika hurejeshewa nauli waliyojia kwa hisani ya shirika la kimataifa llinalojisgughulishaa na masuala ya Afya ya uzazi la Amref.


Aidha,Dk.Mbwanji ameyataja maeneo ya pembezoni kuwa yenye kusumbuliwa kwa kiasi kikubwa na Fistula huku Kwa mkoani Mbeya akizitaja wilaya za Mbozi,Momba na Chunya kuwa zilizo na wagonjwa wanaojitokeza kwa wingi kutibiwa ugonjwa huo.

No comments:

Post a Comment