Naibu waziri wa maji,
Mhandisi Maryprisca Mahundi amewapa sapoti ya vifaa mbalimbali wachezaji soka
wa zamani wa Mwanjelwa Veterani kuelekea Bonanza la maveterani
Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ambalo limepangwa kufanyika Juni tatu na nne mwaka huu.
Kwa mwaka huu mashindano hayo yatafanyika jijini Mbeya kwenye uwanja wa Magereza na uwanja wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya(Must).
Mwenyekiti wa Mwanjelwa
Veterani Ndambi Mwaipopo amesema wao kama wenyeji wa mashindano hayo
wanamshukuru Naibu waziri wa maji Mahundi kwa kuendelea kuwaunga mkono
wachezaji waliocheza soka zamani maarufu kama maveterani ambao wamekuwa
wakikutana mara kwa mara.
“Tunamshukuru sana
Mhandisi Mahundi amekuwa bega kwa bega kusapoti michezo,mabonanza haya
yanatukutanisha wachezaji wakongwe,tunabadilishana uzoefu wa mambo
mbalimbali"amesema Mwaipopo
Mwanjelwa Veterans ndio
mabingwa watetezi wa michuano hiyo ambapo msimu uliopita walifanikiwa kuchukua
ubingwa wa Bonanza hilo ambalo lilifanyika Songea na Ilula.
CREDIT TO SHABAN
NASSORO