Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa miguu mkoa wa Mbeya(MREFA) Sadiki Jumbe amesema mkoa wa Mbeya umejaaliwa vipaji hivyo watahakikisha soka linachezwa kila sehemu...!!
Jumbe ameyasema hayo wakati wa Hafla ya utambulisho wa mashindano ya MO Quality Mbeya Ndondo Cup ambapo amesema kupitia mashindano hayo wanaamini wataibua vipaji ambavyo vitakuwa msaada kwa soka la Tanzania...!
Mashindano ya MO Quality Mbeya Ndondo Cup 2023 yamepangwa kuanza kutimua vumbi June 10,2023 katika uwanja wa shule ya msingi Mwenge ambapo timu 16 zitashiriki michuano hiyo...!!
No comments:
Post a Comment