Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, May 30, 2023

MBEYA KUZIDI KUZALISHA VIPAJI VYA SOKA.

 Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa miguu mkoa wa Mbeya(MREFA) Sadiki Jumbe amesema mkoa wa Mbeya umejaaliwa vipaji hivyo watahakikisha soka linachezwa kila sehemu...!!

Jumbe ameyasema hayo wakati wa Hafla ya utambulisho wa mashindano ya MO Quality Mbeya Ndondo Cup ambapo amesema kupitia mashindano hayo wanaamini wataibua vipaji ambavyo vitakuwa msaada kwa soka la Tanzania...!
""Mkoa wa Mbeya ni wa pili kisoka ukiondoa Dar es Salaam,tuna timu tatu za ligi kuu,tunatamani kuona hizi ndondo zinachochea maendeleo katika soka," amesema Jumbe
Mashindano ya MO Quality Mbeya Ndondo Cup 2023 yamepangwa kuanza kutimua vumbi June 10,2023 katika uwanja wa shule ya msingi Mwenge ambapo timu 16 zitashiriki michuano hiyo...!!




No comments:

Post a Comment