Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, May 20, 2023

HAKUNA MCHEZAJI ANAEDAI MSHAHARA MBEYA CITY


Mstahiki Meya wa jiji la Mbeya Dour Issa Mohamed ambae pia ni mlezi wa klabu ya Mbeya City amesema hakuna mchezaji yoyote anayedai mshahara kama inavyoripotiwa na baadhi ya wadau wa soka...!!

Ameyasema hayo wakati Taasisi ya Tulia Trust ikizindua zoezi la ugawaji wa jezi za mashabiki wa Mbeya City kutoka Kata zote 36 ndani ya jiji la Mbeya kwa lengo la kuhamasisha michezo....!!
""Maneno yamekuwa mengi ,,niwahakikishie wachezaji wamelipwa mpaka mwezi wa nne 2023 hakuna mchezaji anaedai mshahara,hata bonasi zao zote wamelipwa,,wale vijana wanafanya kazi wanafamilia zinawategemea kwaio lazima tuwawekee mazingira mazuri,tunathamini sana jasho lao"" amesema Dour Mohamed..
Hata hivyo ameongeza kuwa wadau na mashabiki wanapaswa kushikimana ili kuhakikisha kikosi chao kinamaliza vizuri michezo yao miwili iliyosalia ya kumaliza msimu wa mwaka 2022/2023 dhidi ya Yanga pamoja na KMC.

No comments:

Post a Comment