Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, May 31, 2023

PRISONS YAPIGA MARUFUKU WACHEZAJI NDONDO CUP

Klabu ya Soka ya Tanzania Prisons imepiga marufuku wachezaji wake kucheza michezo ya ligi za mchangani maarufu kama Ndondo Cup katika kipindi hiki cha kuelekea kumalizika kwa msimu wa ligi kuu ya NBC 2022/23.

 

Ofisa habari wa Prisons, Jackson Mwafulango amesisitiza kuwa ni marufuku wakati ligi ikiwa bado haijamalizika mchezaji wao kuchezea ndondo Cup na kusisitiza kuwa mchezaji yeyote atakaebainika atachukuliwa hatua za kisheria.

 

CREDIT TO SHABAN NASSORO


No comments:

Post a Comment