Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, May 5, 2023

TANZANIA YACHAGULIWA KWA KISHINDO KUWA MAKAO MAKUU YA BARAZA LA MICHEZO AFRIKA KANDA YA NNE


 Na Mwandishi Wetu, Arusha.

 

Nchi Wanachama wa Baraza la Michezo la Umoja wa Afrika Kanda ya IV zimeichagua  Tanzania kuwa  Makao Makuu ya Sekretarieti ya Baraza hilo linaloundwa na nchi 14.

 

Ushindi huo umepatikana kupitia mkutano wa Baraza hilo uliofanyika jana Mei 4, 2023 jijini Arusha chini ya uongozi wa na Mwenyekiti  Mhe. Peter Ogwang ambaye ni Waziri anayeshughulikia masuala ya Michezo nchini Uganda.

 

Tanzania imepitiswa na Wajumbe kutoka Nchi 14 zinazoshiriki Mkutano  huo ambazo ni Comoro, Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Madagascar, Mauritius, Rwanda, Shelisheli, Somalia, Sudan Kusini, Sudan, Uganda na  wenyeji Tanzania.

 

Akizungumza mara baada ya Tanzania kuchaguliwa, Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amewashukuru Wajumbe hao akiwahakikishia kuwa Tanzania itakua tayari kusimamia, kuendeleza na kuhakikisha mipango na matarajio ya Baraza hilo yanafikiwa kwa mafanikio makubwa.

 

Mkutano unaofuata wa Baraza hilo utafanyika Zanzibar Aprili, 2024.

No comments:

Post a Comment