Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, May 30, 2023

KENGOLD KUVUNJA KIKOSI CHOTE, BENCHI LA UFUNDI


Mkurugenzi wa kikosi cha KenGold FC Keneth Mwakyusa Mwambungu amepanga kufanya maboresho makubwa katika timu hiyo kuelekea msimu ujao wa ligi ya Championship...!!

Mwambungu amesema baada ya kumalizika ligi wamefanya tathimini na kubaini mapungufu mbalimbali hivyo wanaanza kuyafanyia kazi mapema....!!
""Unajua ligi daraja la kwanza ni ngumu sana,,tumecheza huu msimu wa tatu sasa,,navunja kikosi chote pamoja na benchi la ufundi,tunaanza upya" Amesema Keneth
Nae Katibu mkuu wa KenGold Benson Mkocha ameongeza kuwa baada ya kushindwa kufikia malengo ya kupanda ligi wameona waanze upya ambapo hivi karibuni wataanza kutangaza utaratibu wa namna gani watafanya usajili...

No comments:

Post a Comment