Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, September 24, 2012

WABAKAJI SASA KUHASIWA

MKAZI wa kata ya Nzovwe,Jijini Mbeya,Rehema Mwamengo (39) amependekeza katika katiba ijayo iwe na sheria ya kuhasiwa sehemu za siri kwa mwanaume yoyote atakaebainika na kuthibitishwa na mahakama kumbaka mtoto wa kike.

Kufuatia pendekezo hilo, umati mzima wa watu uliokuwepo ukisikiliza mkutano huo kuangua kicheko huku wanawake wakionekana kupiga vigelegele na makofi kwa kumsifu mama huyo.

Pendekezo hilo alilitoa mbele ya jopo la wajumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba mpya wakati wa mkutano wa kukusanya maoni toka kwa wananchi juu ya mchakato mzima  wa uundwaji katiba nyingine itakayokuwa imewashirikisha wananchi kote nchini.

Mwamengo alisema kuwa hivi sasa adhabu ya mwanaume anayekutwa na hatia ya kubaka kufungwa jela miaka 30 haitoshi kwa dai kuwa vitendo hivyo bado vinashamili siku hadi siku miongoni mwa jamii.

Alisema kuwa vitendo hivyo licha ya kuwa na adhabu hiyo ya kufungwa miaka 30 jela lakini watoto wanaokuwa wamefanyiwa kitendo hicho hujikuta wakiwa katika hali mbaya ambapo baadhi yao hupata ulemavu sehemu za uzazi.

Aidha, alidai kuwa endapo katiba ijayo itaridhia kuwepo kwa adhabu hiyo ya kuhasiwa kwa mwananume anayekuwa na hatia ya kubaka heshima itakuwepo na itakuwa ni fundisho hata kwa wale wenye tabia ya kupalamia watoto wa kike.

“Nasema hivi mwanaume yoyote atakakaebainika na kuthibitishwa na mahakama kuwa ana hatia hiyo ya kubaka adhabu yake iwe ni kuhasiwa tu ili iwe ni fundisho kwa wanaume wengine”alisema mama huyo na kuongeza:

“Hivi sasa  adhabu ya mwanaume atakaekutwa na hatia kama hiyo kufungwa miaka 30 na adhabu hiyo inatekelezwa na mahakama lakini bado tabia hiyo ipo na inazidi kuwaumiza mabinti zetu, na  hali hiyo  inaashilia kuwa haitoshi kwa mwanaume huyo,hivyo nashauri kwamba adhabu yake iwe ni kuhasiwa tu”alisema.

No comments:

Post a Comment