JUMLA ya shilingi 50,436,000 zimekusanywa katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania bara kati ya timu ya Yanga ya Dar es salaam na Tanzania Prison ya jijini Mbeya uliochezwa jumamosi katika uwanja wa Sokoine jijini hapa.
Katibu wa chama cha soka mkoani Mbeya (MREFA) Lawrence Mwakitalu ametangaza makusanyo hayo yaliyopatikana kwa njia ya viingilio kutoka kwa mashabiki 16,812 waliofika kushuhudia mchezo huo.
No comments:
Post a Comment