Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, November 28, 2012

KIFO CHA MTANGAZAJI CLEMENCE MPEPO


TASINIA ya habari mkoani Mbeya imepata pigo kufuatia kifo cha mtangazaji Clemence Mpepo(Mzee wa Makabila) wa kituo cha redio cha Bomba FM cha jijini Mbeya.

Mpepo alifariki usiku wa kuamkia Novemba 28 mwaka katika hospitali ya taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam alikokuwa amelazwa akiendelea kupata matibabu kufuatia maradhi ya mapafu yaliyokuwa yakimsumbua.

Enzi za uhai wake mtangazaji huyo alijipatia umaarufu mkubwa kwa mashabiki mkoani hapa na maeneo ya jirani kufuatia umahiri wake wa kutangaza kipindi cha nyimbo za asili ambapo alikuwa mtaalamu wa lugha za makabila mbalimbali hali iliyokuwa ikiwavutia wasikilizaji wengi wa kipindi hicho kilichokuwa kikirushwa kila siku ya jumamosi.

Akizungumzia kifo hicho Meneja wa redio Bomba Fredy Helbert alisema ofisi imepokea kifo hicho kwa masikitiko makubwa kutokana na ushirikiano mkubwa aliokuwa nao Mpepo mpaka anaanza kusumbuliwa na maradhi.

Alisema marehemu alianza kuugua siku chache baada ya kufunga ndoa hivi karibuni akiwa bado katika likizo ya ndoa na baadaye hali ilizidi kuwa mbaya na kulazwa katika hospitali ya Mkoa na hatimaye Rufaa Mbeya kabla ya kupelekwa Muhimbili.

“Alikuwa bado katika likizo ya ndoa hivyo hata kazini alikuwa hajaanza kuingia ndipo maradhi yalipoanza kumsumbua.Jambo lililokuwa likitupa matumaini kuwa mpaka anaondoka na mkewe kwenda Dar es salaam alikuwa na unafuu mkubwa.Alikuwa akizungumza vizuri na kucheka nasi kama tulivyokuwa tumemzoea.Ghafla tukapata taarifa hali imebadilika na leo tunazungumza msiba”.

“Ni masikitiko makubwa kwetu kama wafanyakazi wenzake.Hakuwa mtu wa kukorofishana na mtu.Mcheshi wakati wote Lakini kikazi pia japo siku hizi watu wanasema pengo linazibika kwa Mpembo kwakweli ni vigumu maana utangazaji wake ulikuwa si wa kipindi kimoja.Kila kipindi tulichompa kilipata wasikilizaji wengi” alisema.

Kwa mujibu wa meneja huyo Mpepo atazikwa siku ya jumamosi Kinyelezi jijini Dar es salaama kutokana na maamuzi ya wazazi wake.

No comments:

Post a Comment