Saturday, April 6, 2013
WATANZANIA WATAKIWA KUJIVUNIA KUMILIKI ZIWA NYASA
TANZANIA huchangia asilimia 59 ya maji ya ziwa Nyasa kupitia mito yake
kiasi ambacho ni kikubwa ikilingaanishwa maji kutoka nchi za Malawi na
Msumbiji.
Hayo yalibainishwa na Ofisa wa maji Bonde la ziwa Nyasa Witgal
Nkondola alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Nkondola amesema nchi jirani ya Malawi inachangia asilimia 33 ya maji
ya ziwa hilo huku asilimia nane zinazosalia zikichangiwa na mito
iliyopo nchini Msumbiji.
Hata hivyo ofisa huyo amesema ni watanzania wachache wanaotambua kuwa
mitoaa yao inachangia kwa kiasi kikubwa maji ya ziwa hilo hivyo
wanapaswa kujisikia fahari kuwa sehemu ya wamiliki wa ziwa hilo.
Almeitaja mito ya Songwe,Kiwira na Lufilyo iliyopo mkoani Mbeya kuwa
miongoni mwa mito inayoingiza maji kwa wingi katika ziwa hilo.
Amekiri pia vivutio vya utalii vilivyopo kwenye ziwa hilo na eneo zima
la Bonde la Maji la Ziwa Nyasa kutotangazwa ipasavyo yakiwemo maziwa
madogo ya asili 11 yaliyopo wilayani Rungwe.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment