Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, May 3, 2013

JAMBAZI WATANO WAUAWA

MAJAMBAZI watano wameuawa kwa kupigwa risasi katika majibizano ya risasi kati yao na polisi mkoani Mbeya. Kuuawa kwa majambazi hao wasiofahamika majina wala makazi yao kunatokana na taarifa zilizolifikia jeshi la polisi na kuanza kuzifanyi kazi tangu asubuhi ya leo Mei 3). Kamanda wa polisi mkoani hapa Diwan Athuman aliwaambia waandishi wa habari kuwa jeshi hilo lilikuwa na wakati mgumu kufuatilia taariza za waharifu hao kwakuwa haikujulikana walikuwa wapi. Kamanda Athuman amesema hatimaye mnamo majira ya saa sita mchana askari waliokuwa katika eneo la Garijembe barabara ya Mbeya/Tukuyu walisimamisha gari yenye namba T 911 BUG aina ya Toyota Spacio kwa lengo la kuikagua na ndipo ghafla walishuka watu watano wawili kati yao wakiwa na bunduki na kuanza kufyatua hovyo risasi. Amesema hali hiyo ilisababisha askari waliokuwa eneo hilo kuanza kujibu mashambulizi na ndipo walipofanikiwa kuwajeruhi majambazi hao na walipowafikisha hospitali ya rufaa wakawa wamefariki dunia. Ametaja vitu vilivyokamatwa kuwa ni pamoja na gari waliyokuwa nayo jambazi,bunduki mbili moja ya kivita aina ya Sub Machine Gun(SMG) iliyokuwa na risasi 16 zilizokuwa zimesalia na nyingine aina ya Mark III ikiwa na risasi mbili zilizosalia. Ndani ya gari hiyo pia ilikutwa kama moja ngumu ambayo haikufahamika ilikuwa kwaajili ya shughuli ipi. Amewataka wananchi mkoani hapa kufika katika hospitali ya rufaa kuweza kutambua miili ya jambazo hao waliokufa kutokana na kujeruhiwa maeneo mbalimbali ya miili yao kwa risasi.

No comments:

Post a Comment