Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, May 15, 2013

WALIOKUFA KWENYE AJARI YA GARI JANA MBEYA HAWA HAPA

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Mbeya Diwani Athuman waliokuwa kwenye ajali ya gari jana eneo la Mwansekwa ni Filimon Mgumbe(30) mkulima na mkazi wa Itigi na Baraka Mwasota(24) mkazi wa Mwansekwa. Amesema mtu wa tatu ambaye ni mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 25-30 hakufahamika jina wala makazi yake na kuwataka wananchi kufika katika hospitali ya rufaa kuutambua mwili wake. Amewataja waliojeruhiwa kuwa ni pamoja na wawili ambao walipatiwa matibabu na kuruhusiwa kuondoka ambao maji yao hayakutambuliwa lakini wawili bado wamelazwa katika hospitali ya rufaa. Wanaoendelea kupata matibabu ni pamoja na raia wa China Don Fung Cheng(38) na mwanaume mmoja ambaye hajatambulika jina wala makazi yake kwakuwa hawezi kuzumngumza.

No comments:

Post a Comment