Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, May 28, 2013

COCA COLA WAPANIA KUCHEZA LIGI KUU

Meneja wa kiwanda cha Coca Cola Kwanza cha mkoani Mbeya Gary Pay akiwa amembeba mmoja wa wafanyakazi wa kiwanda hicho ikiwa ni moja ya michezo iliyofanyika kwenye hafra ya kusherehekea kombe la mashindano ya kombe la Mkurugenzi mkuu wa Coca Cola nchini lililofahamika kama MD Cup 2013 ambapo timu ya Coca Cola kwanza waliibuka mabingwa na kukabidhiwa kombe hilo. KIWANDA cha vinywaji baridi cha Coca Cola Kwanza cha mkoani Mbeya kimeelezea nia yake ya kuwa na timu itakayoshiriki mashindano makubwa nchini ikiwemo ligi kuu ya Tanzania bara. Meneja wa kiwanda Gary Pay alieleza nia hiyo kwa wafanyakazi wake waliohudhuria hafra ya kusherehekea kombe la mashindano ya kombe la Mkurugenzi mkuu wa Coca Cola nchini lililofahamika kama MD Cup 2013 ambapo timu ya Coca Cola kwanza waliibuka mabingwa na kukabidhiwa kombe hilo. Pay alisema kampuni ya Coca Cola kupitia kiwanda hicho iko katika mkakati wa kuhakikisha wanaismarisha timu hiyo na kuiwexzesha kushiriki mashindano makubwa. Alisema ili kutekeleza nia hiyo tayari kampuni imeingia mkataba wa mwaka mmoja na kocha Charles Makwaza atakayekuwa akiinoa kwa muda huyo na tayari wameanza mchakato wa kuisajili na kuiwezesha kushiriki michuano kwa ngazi mbalimbali ili kuanza kupanda daraja. “Sisi tunalinganisha uwepo wa timu sawa na utendajui katika kiwanda chetu.Tukiitazama safu ya ushambuliaji ni sawa na safu yetu ya mauzo,kwa upande wa safu ya ulinzi ni sawa na kitengo cha uzalishaji kiwandani.Kwa ujumla timu yote ni sawa na watumishi wote pale kiwandani.Hii ni sehemu ya mafanikio yetu kibiashara” “Tumedhamiria,tumeamua na tunaamini tutafanikiwa siku moja kuwa na timu itakayokuwa na upinzani mkubwa kwa timu nyingine nchini kwenye mashindano makubwa hususani ligi kuu” alisema. Naye kocha Makwaza alisema aliipongeza kampuni hiyo kwa kutambua uwezo wake na kumpa mkataba wa kuifundisha timu hiyo huku akiahidi kuhakikisha kikosi chake kinakuwa tishio kwa timu nyingine ili kutimiza malengo ya kuanzishwa kwa timu. Kwa upande wake nahodha wa timu hiyo Bahati Jonas alisema ushirikiano wa karibu baina ya wachezaji na uongozi wa kampuni ni miongoni mwa mambo yatakayoiwezesha kufikia malengo yanayotarajiwa

No comments:

Post a Comment