Mgeni rasmi Afisa
Utalii Tanapa Nyanda za juu kusini Risala Kabongo(katikati) akiwa na wanachama wa kikundi cha uhifadhi wa Mazingira Kihesa Kilolo( KIUMAKI) kwenye uzinduzi wa utalii wa ndani uliofanyika kwenye jiwe Igereke mkoani Iringa
Jiwe Igereke liko katika Mtaa wa Kihesa Kilolo manispaa ya Iringa
mkoani Iringa.Eneo hilo linasimamiwa na kikundi cha uhifadhi wa
Mazingira Kihesa Kilolo( KIUMAKI).Lengo la uzinduzi wa utalii huu wa ndani ni kuwahimiza wananchi wa Iringa kutembelea
vivutio vyao.
Katika uzinduzi huo pia Tanapa walikabidhi mipira kwaajili ya mchezo wa mpiara wa miguu kwa wanakikundi ili kuimarisha michezo na pia ushirikiano.
No comments:
Post a Comment