Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, September 18, 2015

UZINDUZI WA UTALII WA NDANI KATIKA JIWE IGEREKE IRINGA

Mgeni rasmi Afisa Utalii Tanapa Nyanda za juu kusini Risala Kabongo(katikati) akiwa na wanachama wa kikundi cha uhifadhi wa Mazingira Kihesa Kilolo( KIUMAKI) kwenye uzinduzi wa utalii wa ndani uliofanyika kwenye jiwe Igereke mkoani Iringa

Jiwe Igereke liko katika Mtaa wa Kihesa Kilolo manispaa ya Iringa mkoani Iringa.Eneo hilo linasimamiwa na kikundi cha uhifadhi wa Mazingira Kihesa Kilolo( KIUMAKI).Lengo la uzinduzi wa utalii huu wa ndani ni kuwahimiza wananchi wa Iringa  kutembelea vivutio vyao.

Maafisa wa Tanapa wakiwa na wanakikundi chini ya jiwe Igereke.


Katika jiwe hili kuna michoro ya kale kama ile ya Kondoa.Inasemekana ilichorwa na binadamu wa kale.
 

 



 
Katika uzinduzi huo pia Tanapa walikabidhi mipira kwaajili ya mchezo wa mpiara wa miguu kwa wanakikundi ili kuimarisha michezo na pia ushirikiano.

No comments:

Post a Comment