Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, September 21, 2015

IBADA YA KUWEKWA WAKFU ASKOF PANJA WA KANISA LA MORAVIAN

Maaskofu mbalimbali wakiwa mwombea kwa kumpa baraka Askofu wa kanisa la Moravian Jimbo la kusini mchungaji Kenan Panja kwenye ibada maalumu ya kuwekwa wakfu askofu huyo iliyofanyika jumapili mjini Tukuyu wilayani Rungwe.
 Makamu wa Rais Dk.Mohamed Gharib Bilali akisalimiana na maaskofu mara baada ya kuwasili uwanjani kwaajili ya ibada


Wachungaji mbalimbali wa kanisa la Moraviana wakiwa katika ibada





 Mwenyekiti wa kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji Samwel Kabigi akisoma risala ya kanisa mbele ya mgeni rasmi makamu wa Rais Dk.Bilali.
 Kwaya ya  Shalom ikitumbuiza katika ibada hiyo maalumu mbelea ya makamu wa Rais Dk.Bilali.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akitoa salamu za mkoa kabla ya kumkaribisha makamu wa Rais Dk.Bilali
 Makamu wa rais Dk.Mohamed Gharib Bilali akimpongeza askofu Panja kwa kufikia daraja hilo la kiroho.Numa ya askofu na mkewe mama Panja.
 Makamu wa Rais Dk.Bilali akihutubia waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria ibada hiyo ya kuwekwa wakfu kwa askofu Panja.
  Askofu Panja akitoa neno la Shukrani mara baada ya kuwekwa wakfu.



No comments:

Post a Comment