Mtu mmoja mkazi wa kijiji cha
Isandula kata ya Kilimampimbi wilayani Mbozi mkoani Songwe ameuawa kwa kukatwa
mapanga na watu wasiofamika.
Diwani wa kata ya Kilimampimbi
Henry Mwilenga akizungumza na mwandishi wetu kwa njia ya simu amemtaja marehemu kuwa ni Luka Kabuka
anayekadirwa kuwa na umri wa kati ya miaka 70-80 mkazi wa Isandula wilayani
humo
Mwilenga amesema tukio hilo limetokea march 21
saa mbili usiku mwaka huu ambapo marehemu alikuwa akitokea matembezini na kabla
hajafika nyumbani kwake mita sabini alivamiwa na watu wasiofahamika na
kufanyiwa unyama huo.
Amesema tukio hilo limegunduliwa na
mtoto wa marehemu ambaye naye siku ya tukio alichelewa kufika nyumbani na
wakati anafika karibu na eneo la tukio ndipo aligunduwa kuwa aliyeuawa ni baba
yake na ndipo akapiga mayowe na kuomba msaada.
Mwilenga amesema baada ya tukio
hilo kutokea waliuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka hospitali ya wilaya ya
mbozi kwaajili ya uchunguzi na kusadikiwa kuwa marehemu alinyofolewa baadhi ya
viungo na wakuruhusiwa kwa ajili ya mazishi.
Katika hatua nyigine diwani huyo
amesema marehemu ameuauwa kinyama kwani alipoingalia maiti ilikutwa na majereha
makubwa matano usoni hali inayoashiria kuwa alipigwa na vitu vyenye ncha kali.
Aidha amewataka wananchi kutoa
ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuwagundua watu waliohusika na unyama huo
kwani tukio hilo ni la pili kutokea katika kata hiyo ndani ya miaka miwili.
No comments:
Post a Comment