Na Joachim Nyambo.
AMA kweli safari ni hatua!Ndiyo
maneno yanayoweza kutumiwa na wadau wa elimu ndani na nje ya nchi
wanapokizungumzia Chuo kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya(MUST).Chuo hiki
kilianzishwa rasmi 2012 baada ya mabadiliko ya iliyokuwa Taasisi ya Sayansi na
Teknolojia Mbeya(MIST).Kilikabidhiwa Idhini ya chuo kikuu mwaka 2013.
Tangu kupewa idhini hiyo tayari Chuo
tayari chuo hiki kimeendesha mahafali tatu zenye kudhihirisha jitihada zake
katika kuendeleza na kutoa fursa za kitaaluma kwa maendeleo ya jamii mbalimbali
nchini.Hadi mwishoni mwa mwaka jana tayari wahitimu 2,297 wametunukiwa
stashahada na shahada mbalimbali chuoni hapa tangu kipandishwe hadi na kuwa
chuo kikuu.
Katika mahafali ya tatu ya chuo
hicho yaliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana,makamu mkuu wa chuo,Prof Joseph
Msambichaka alisema mafanikio yaliyopo na yanayoendelea kutokea ni matokeo ya
ushirikiano mzuri baina ya uongozi wa Must na serikali katika ngazi mbalimbali.
“Mafanikio yoyote ya kitaasisi huja
kutokana na ushirikiano mzuri unaokuwepo baina ya wadau mbalimbali.Hata
mafanikio haya tunayoyazungumzia ya kutunuku shahada kwa idadi hii kubwa ya
wanafunzi ni matokeo ya ushirikiano mzuri.Na huu ni mhimili muhimu utakaozidi
kukipa mafanikio makubwa na mazuri chuo chetu siku za usoni”
Prof Msambichaka anasema kwa
kuzingatia mahitaji ya uboreshaji wa elimu ya sekondari nchini kupitia mpango
wa Maendeleo wa Elimu ya Sekondari(MMES) ambao umesaidia sana kuongeza idadi ya
shule za sekondari nchini na pia mkakati wa kujenga maabara za sayansi katika
kila sekondari,chuo hicho kinaandaa mitaala ya kufundishia shahada ya ualimu wa
masomo ya sayansi ili kulisaidia taifa kupata walimu wa kutosha katika masomo
hayo
Anasema chuo pia kinaendelea na
mipango ya kuanzisha Chuo cha Mafunzo ya Ualimu na Sayansi(College of Science
and Education) kitakachokuwa mahususi kwaajili ya kutoa mafunzo ya ualimu
katika masomo ya Sayansi ambapo mafunzo hayo yataanza kutolewa katika mwaka wa
masomo 2016/2017.
“Must pia imeandaa mitaala mipya
kwaajili ya kutolea mafunzo uhandisi katika ngazi za Stashahada ya juu ya
mafuta na gesi na uhandisi Ujenzi,Shahada ya uzamili ya uhandisi nishati
mbadala na uhandisi maji na ujenzi na Shahada ya uzamivu ya uhandisi maji na ya
uhandisi Ujenzi.Mafunzo haya pia yataanza mwaka wa masomo ujao” alisema Prof
Msambichaka.
Anasema udahili wa wanafunzi kwa
mwaka 2014/2015 ulikuwa na wanafunzi 3,342.Jitihada za kuanzishwa Chuo cha
Mafunzo ya Ualimu na Sayansi,kuanzishwa Kampasi mpya mkoani Rukwa na kuendelea
kuanzisha kozi mpya katika chuo cha teknolojia na uhandisi kunategemewa
kuongeza udahili wa wanafunzi mpaka kufikia wastani wa wanafunzi 4,000 katika
mwaka wa masomo 2016/2017.
“Chuo kimeendelea kutoa mafunzo ya
awali yaani Pre entry course ili kuwawezesha wanafunzi wa kike wasiokuwa na
ufaulu wa kutosha kujiunga na mafunzo ya stashahada za uhandisi na teknolojia
katika fani mbalimbli.”
“Katika mwaka wa masomo 2015/2016
wanafunzi wa kike 42 waliweza kufaulu na hivyo kuwa na sifa za kujiunga na
mafunzo ya stashshada katika fani za uhandisi na teknoloji”
Kuanzishwa kwa mafunzo ya Lugha ya
kichina ni mafanikio mengine ya chuo hiki kinachozidi kupaa kimaendeleo.Hii ni
sehemu ya kuendeleza ushirikiano baina ya chuo hicho na vyuo vingine duniani.
Kwa mujibu wa Prof Msambichaka
mafunzo ya lugha ya Kichina yalianza kutolewa Novemba mwaka huu na yanafanyika
kwa ushirikiano baina ya Must,Chuo kikuu cha Dar es salaam na Taasisi ya
Confucius ya nchini China.Kuanza kutolewa kwa mafunzo ya lugha ya kichina ni
fursa kwa wafanyabiashara na wanafunzi kujifunza lugha hiyo ili kupanua wigo wa
mawasiliano na biashara kimataifa hasa ikizingatiwa kuwa China inaendelea kwa
kasi kubwa sana kiuchumi.
Akizungumzia uboreshaji wa utoaji
taaluma chuoni hapo,Makamu mkuu huyo wa chuo anasema uendelezaji wa kitaaluma
kwa watumishi unaendelea kufanyika lengo likiwa ni kuwezesha upatikanaji wa
uhakika wa rasiliamli watu.
Chuo kimeendelea kusomesha watumishi
katika ngazi mbalimbali ambapo kwa sasa kina jumla ya watumishi 68 walioko
masomoni ambao kati yao 43 ni walimu na miongoni mwa walimu hao 15 ni wa
shahada ya uzamivu na 28 shahada ya Uzamili.Waendeshaji mitambo ni 25 ambao
shahada ya uzamili wapo sita,Shahada ya kwanza 13 na stashahada wapo sita.
“Chuo pia kwa kushirikiana na
kampuni ya RAINAT Technical Solution imeweza kuanzisha maktaba ya mtandaoni
kwaajili ya kuwawezesha wanafunzi wa ngazi mbalimbali nchini kuweza kusoma
vitabu mtandaoni”
“Tovuti ya maktaba hiyo ya www.tovl.ac.tz ambayo kwa sasa iko katika
majaribio itazinduliwa mapema wakati wowote” anabainisha Prof Msambichaka.
Pamoja na mafanikio ambayo chuo
kimepata katika kipindi cha mwaka 2014/2015,chuo kina mipango mbalimbali ili
kukabili changamoto zilizopo na zitakazojitokeza baadae.Kuongeza udahili wa
wanafunzi hususani kwa wanafunzi wa kike ni miongoni mwa mipango husika.
Chuo kina mpango wa kusomesha
watumishi wengi zaidi hasa katika ngazi ya shahada ya uzamivu.Kuwezesha
ufanyikaji wa tafiti zenye kutatua changamoto za kiuchumi na kijamii,Kuongeza
vitabu na nafasi katika maktaba na kuongeza mitambo na vifaa vya kufundishia
katika karakana na maabara.
Kuna mpango wa kuongeza majengo ya
madarasa,maabara na karakana,mabweni ya wanafunzi,numba za kuishi
watumishi,kukarabati na kuboresha mifumo ya maji machafu,maji masafi na umeme
na pia kukarabati na kuboresha barabara za ndani ya chuo na kuendelea
kuwasiliana na halmashauri ya jiji la Mbeya kujenga barabara inayounganisha
chuo na barabara kuu ya Mbeya-Tunduma.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza
la Chuo Prof Penina Mlama anasema pamoja na mafanikio yaliyopo bado kuna
changamoto kubwa katika udahili wa wanafunzi wa kike.Anasema jitihada zaidi
zinahitajika katika kuhamasisha jamii juu ya suala hilo.Huenda mfumo dume bado
ni tatizo linalokwamisha jamii ya wanawake kujiunga na chuo hicho.
Hata hivyo Prof Mlama anasema
kupitia utendaji kazi wa serikali ya awamu ya tano chini ya utawala wa rais Dk
John Magufuli chuo kitaweza kufanya mambo makubwa zaidi.Iwapo katika kipindi
cha miaka michache tangu kipewe hadhi ya chuo kikuu kimeweza kutoa zaidi ya
wahitimu 2000 basi kwa miaka ijayo mafanikio makubwa yatarajiwe.
Anaahidi chuo hicho kutekeleza
majukumu yake kwa ufanisi wenye kuzingatia falsafa muhimu ya Hapa Kazi Tu
akisema ni yenye malengo ya kulijenga taifa na watu wake kwa ujumla.
No comments:
Post a Comment