Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, November 6, 2014

GEPF YATINGA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI

 Meneja Masoko wa GEPF Aloyce Ntukamanzina akizungumza jambo katika kikao cha maafisa wa mfuko huo,wanahabari na wadau wengine





MFUKO wa Mafao ya Kustaafu(GEPF) umetajwa kukua kwa kasi katika kipindi cha miaka 10 iliyopita na kuwezesha kuzidi kuongeza matawi nchini ili kuwafikia wateja wengi zaidi.

Tayari GEPF imefungua tawi lake mkoani Mbeya na litakuwa likitoa huduma za mafao yake kwa wateja walioko katika mikoa ya kanda ya nyanda za juu kusini.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa ofisi za mkoani Mbeya zilizopo eneo la uhindini,Meneja Masoko wa GEPF Aloyce Ntukamanzina alisema wanachama wa mfuko huo wameongezeka kutoka 16,131 mwaka 2004 na kufikia 76,000 mwaka 2014.

Ntukamanzina amesema mwaka 2004 mfuko huo uliweza kukusanya shilingi bilioni 5.1,lakini mwaka huu umeweza kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 37.29.


Meneja Masoko huyo amesema mafanikio hayo yanatokana na sababu mbalimbali ikiwemo uongozi bora na uwekezaji makini sambamba na mabadiliko ya mfumo wa kiutendaji.

Amesema ujio wa GEPF ni fursa nyingine kwa wakazi wa mkoa wa Mbeya,ya kujiwekea hazina ya mafao ya uzeeni ili watakapokuwa na umri usiwawezesha kufanya shughuli za uzalishaji mali waweze kuendelea kuishi maisha bora kama hapo awali.

Amesema bado kuna changamoto ya watanzania wengi kutopenda kujiunga na mifuko ya hifadhi za jamii jambo alilosema limekuwa likisababisha watu wengi kuishi maisha magumu mara wanapozeeka na kukosa nguvu za kufanya kazi za uzalishaji mali.

No comments:

Post a Comment