Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, August 15, 2014

MBEYA CITY,TANZANIA PRISONS WAZUIWA KUTUMIA UWANJA WA SOKOINE

KIKOSI CHA MBEYA CITY
KIKOSI CHA TANZANIA PRISONS

 
WAMILIKI wa Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya wameendelea na jitihada za kuukarabati uwanja huo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya michuano ya ligi kuu ya Tanzania bara itakayoanza kutimua vumbi Septemba 20 mwaka huu.

Ukarabati unaoendelea hivi sasa katika uwanja huo utakaotumiwa na Timu za Mbeya City na Tanzania Prison kama uwanja wa nyumbani ni pamoja na kuondoa magugu yasiyohitajika katika eneo la kuchezea maarufu kama Pichi.

Akizungumza na Lyamba Lya Mfipa,Meneja wa Uwanja huo Modestus Mwaluka amebainisha namna shughuli nzima ya kuondoa magugu hayo inavyoendeshwa,shughuli ambayo pia imesababisha Timu za Mbeya City na Tanzania Prison kuzuiwa kuendelea kuutumia uwanja huo kwa mazoezi.

Mwaluka amesema wanalazimika kuyaondoa magugu hayo kutokana na asili yake mbaya ambapo huweka nundu nundu uwanjani na kusababisha mpira kukosa mwelekeo unaopaswa wakati ukichezwa katika uwanja husika.


Amezitaka timu za Mbeya City na Tanzania Prisons kutojawa na hasira baada ya kuzuiwa kutumia uwanja huo kwa mazoezi badala yake watambue kuwa  uongozi wa uwanja una nia ya dhati ya kuboresha miundombinu itakayosaidia timu hizo kucheza mpira mzuri na wenye kuvutia.

No comments:

Post a Comment