Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, May 22, 2015

TMA YAPELEKA HUDUMA ZIWA NYASA

Mkuu wa wilaya ya Kyela Thea Ntara(wa tatu kutoka kulia) akiwa na maafisa wa TMA na wadau wengine wa shughuli za kimaendeleo katika ziwa Nyasa.Wadau hawa walikutana mjini Kyela kupashana habari za ujio wa TMA katika ziwa Nyasa sambamba na kupeana uzoefu juu ya majanga ya ziwa hilo.
 Kaimu mkurugenzi wa huduma za ufundi za TMA Dk.Pascal Waniha akielezea namna TMA ilivyoona umuhimu wa kufikisha huduma zake kwa watumiaji wa ziwa Nyasa.
 Wadau mbalimbali wa ziwa Nyasa wakiwemo wavuvi wakishiriki semina ya kupeana uzoefu juu ya majanga ya ziwa hilo. 


 Wanahabari kama anavyoonekana mwandishi wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo Solomon Mwansele ni miongoni mwa wadau ambao wametajwa kuwa na umuhimu mkubwa kwenye usambazaji wa taarifa zitakazotolewa na TMA juu ya utabiri wa hali ya hewa ndani ya ziwa Nyasa.
 Mkuu wa wilaya ya Kyela Thea Ntara akibainisha namna ujio wa TMA katika ziwa Nyasa ulivyoleta neema kwa watumiaji wa ziwa hilo


Mkurugenzi wa huduma za Utabiri za TMA Dk.Hamza Kabelwa akibainisha mikakati ya TMA katika utoaji taarifa za hali ya hewa.

                            HABARI KAMILI.

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA) imepeleka huduma zake katika wilayani Kyela lengo ni kusogeza huduma ya upatikanaji wa taarifa za hali ya hewa kwa watumiaji wa ziwa Nyasa.

Kwa mujibu wa watumiaji wa ziwa Nyasa wakiwemo wavuvi na wasafirishaji,kwa muda mrefu wamekuwa wakilazimika kutumia njia za asili kubaini majanga yanayoweza kutokea ndani ya ziwa hilo na wakati mwingine walilazimika kutumia taarifa zilizotolewa na mamlaka ya hali ya hewa ya nchi jirani ya Malawi.

Wakazi wilayani Kyela wanasema kutokana na changamoto hiyo madhara makubwa yamekuwa yakitokea ikiwemo vifo vya wavuvi kutokana na vimbunga vilivyowakumba wakati wakiendelea na shughuli zao ndani ya ziwa Nyasa.

Kaimu mkurugenzi wa huduma za ufundi za TMA Dk.Pascal Waniha anasema mamlaka hiyo imeamua kuwafikia watumiaji wa ziwa Nyasa kutokana na mahitaji yaliyopo.

Mkuu wa wilaya ya Kyela Thea Ntara anasema sasa watumiaji wa ziwa hilo wako katika mazingira salama kwakuwa kabla ya kufanya shughuli zao watapataa taarifa za uhakika juu ya utabiri wa hali ya hewa.

No comments:

Post a Comment