Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, May 26, 2015

MAJIMBO YA MBEYA KUGAWANYWA.



MAJIMBO ya Mbeya mjini na Mbeya vijijini huenda yakagawanywa na kuwa majimbo mawilimawili iwapo Tumea ya taifa ya uchaguzi itaridhia maombi yaliyopendekezwa na wadau kwenye vikao vya Ushauri vya wilaya vilivyofanyika jana.

Vikao vya kuyagawa majimbo hayo vimefanyika kwa nyakati na tofauti kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya ambapo kwa jimbo la Mbeya mjini wadau wamependekeza kuundwa kwa majimbo mapya ya Iyunga na Sisimba huku Jimbo la Mbeya vijijini likipendekezwa kuundwa kwa majimbo ya Mbeya na Isangati.

Akizungumza kwenye kikao cha Ushauri cha wilaya,Mkurugenzi wa jiji la Mbeya Bwana Musa Zungiza amesema mapendekezo ya mgawanyo wa jimbo la Mbeya mjini yanazingatia maeneo ambayo awali yalikuwa ni tarafa.

Bw.Zungiza amesema katika Tarafa ya Iyunga ambayo sasa inapendekezwa kuwa jimbo kuna kata 21 na mitaa 116,iinakadiriwa kuwa na wakazi 327,122 hadi kufikia Julai 2015 idadi aliyosema inakidhi vigezo vya tarafa hiyo kuwa jimbo.

Kwa upande wa tarafa ya Sisimba inayopendekezwa kuwa jimbo la Sisimba amesema ina kata 15 inayokadiriwa kuwa na wakazi 106,264 kufikia Julai mwaka huu.

Naye mkurugenzi mtendaji wa halmashauri Bibi Upendo sanga amesema jimbo la Mbeya litakuwa na kata 11 zinazokadiriwa kuwa na jumla ya wakazi 107,349.

Bi.Sanga amesema jimbo la Isangati lenye kata 15 zinazokadiriwa kuwa na jumla ya wakazi 221.

 Mwisho.


No comments:

Post a Comment