Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, September 24, 2011

Wanafunzi acheni siasa,zinashusha taaluna yenu


Hatua ya vijana walioko mashuleni na vyuoni kujiingiza katika siasa imetajwa kuwa ugonjwa mbaya unaohatarisha taaluma nchini pamoja na mustakabali wa maisha ya watanzania miaka michache ijayo.
Ili kuepuka na balaa linaloweza kuikumba nchi badae vijana hao wametahadharishwa kutojiuhusisha na siasa na badala yake waelekeze nguvu zao kwenye masomo ili kuinua kiwango chao cha Taaluma.
Mwenyekiti wa Chama cha Kuweka na kukopa (Saccos) cha Walimu wa shule za Sekondari wilayani Mbeya, Frank Phiri ameyasema hayo kwenye mahafari ya pili ya kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Itebwa ambapo jumla ya wanafunzi 86 wamehitimu.
Amesema wanafunzi wanapaswa kutambua kuwa viongozi wakisiasa wakongwe wanaowashabikia hivi sasa walijiingiza katika siasa hiyo baada ya kutoka masomoni na si wakiwa masomoni na ndiyo maana taaluma zao zinaonekana kuwa nzuri.
Awali Mwalimu Mkuu wa  shule, Mpege Mwamkota amesema shule hiyo inakusudia kuboresha  huduma za hosteli ili kukabiliana na changamoto ya wanafunzi wa kike kukatisha masomo kutokana na kupata mimba.

No comments:

Post a Comment