Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, January 16, 2012

Maghembe apata kigugumizi suala la kahawa mbichi,alazimika kuheshimu maamuzi ya halmashauri na serikali ya mkoa

Waziri wa Kilimo chakula na ushirika Profesa Jumanne Maghembe amemaliza mgogoro uliodumu kwa muda mrefu wilayani Mbozi kuhusu ununuzi wa kahawa mbichi akisema maamuzi ya halmashauri na serikali ya mkoa kukataa ununuzi huo yanapaswa kuzingatiwa.

Profesa Maghembe ametoa tamko hilo leo (Januari 16) wilayani Mbozi katika mkutano ulioshirikisha wadau wa zao kahawa kutoka halmashauri nne za wilaya ya Mbeya vijijini,Ileje,Rungwe na Mbozi.

Mkutano huo uliokuwa na mvutano mkubwa baina ya pande pili ukiwema unaotetea na ule unaopinga ununuzi wa kahawa mbichi ulianza kwa taarifa za maendeleo ya kilimo cha zao hilo ambapo mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbasi Kandoro amesema ununuzi huo unamnyonya mkulima kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi Eliki Ambakisye ameilaumu wizara kwa kuendelea kuufumbia macho mgogoro huo ili hali inatambua hakuna sheria wala kanuni ya zao hilo inayoruhusu ununuzi wa kahawa mbichi.

Akijibu hoja hizo na nyingine nyingi zilizotolewa na wajumbe Profesa Maghembe amesema wizara haiwezi kutupilia mbali maamuzi ya halmashauri pamoja na serikali ya mkoa hivyo iwapo vyombo hivyo havikubaliani na ununuzi huo lazima maamuzi yazingatiwe.

No comments:

Post a Comment