Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, January 26, 2012

MWANAFUNZI KIZIMBANI KWA WIZI

MWANAFUNZI wa sekondali ya Iramba mkoani hapa,Christina Nyingi(20) amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa kwa kosa la wizi wa mali yenye thamani ya shilingi milioni 2.

Awali, akisomewa mashitaka na wakili wa serikali Adolf Maganda Mbele ya hakimu mkazi Francis Kishenyi alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa novemba 28mwaka jana katika maeneo ya uhindini jijini hapa.

Maganda alieleza mahakamani hapo   kuwa mshitakiwa novemba 28 mwaka jana maeneo ya uhindini aliiba camera ya digital moja,simu  moja aina ya nokia,magauni mawili,chupa sita za pafyumu na mabegi mawili vyote vikiwa na thamani ya milioni 2 mali ya Mili Maboko.

Mshitakiwa alikana shitaka na kurudishwa rumande  katika gereza la Ruanda jijini hapa,baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana na kwamba kesi hiyo itatajwa tena febuari 8 mwaka huu.

Wakati huohuo Mkazi wa Manzese Darajani jijini Dar es salaamu amefikishwa mahakamani hapo akikabiliwa na shtaka la kujifanya polisi.

Akisomewa  shitaka na wakili wa serikali Adolf Maganda mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa Kussaga Majinge alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa  januari 4 mwaka huu katika maeneo ya iyunga mkoani hapa.

Mshitakiwa alikana shtaka na kurudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza Masharti  ya dhama, kesi hiyo itatajwa tena febuari 8 mwaka huu.
 Joachim Nyambo, Mbeya Januari 26 2012

No comments:

Post a Comment