Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, January 21, 2012

Rungwe waunda kamati kufufua CHF

WILAYA ya Rungwe mkoani Mbeya imeunda kamati ndogo ya watu 10 itakayoandaa mikakati ya kuhakikisha hamasa ya mfuko wa afya ya jamii CHF inatolewa kwa wananchi ili waweze kujiunga kwa wingi.

Mpango huo unatokana na wilaya kuwa ya kwanza kwa uhamasishaji huko katika miaka ya nyuma lakini kwa sasa inaonekana kushuka kwa kiasi kikubwa hali inayoonekana kusababishwa na kudorola kwa uhamasishaji.

Kamati hiyo iliundwa jana na mkuu wa wilaya Jackson Msome aliyekubaliana na wadau wengine waliohudhuria mkutano wa wakuu wa Idara za halmashauri hiyo wa kupata taarifa za maendeleo ya CHF na pia kujadili mradi mpya wa kuwasaidia wanawake wajawazito wasio na uwezo kupata huduma za matibabu chini ya utaratibu wa mfuko wa taifa wa bima ya afya NHIF.

Msome amesema ili kuhamasisha wananchi kujiunga kwa wingi ni lazima mikakati madhubuti iwekwe ikiwemo utoaji elimu kwa wakazi juu ya kuwa na bima itakayowahakikishia huduma ya afya pale wanapopata matatizo ya magonjwa.

Kamati iliyoundwa itakayokuwa chini ya mwenyekiti ambaye ni mganga mkuu wa wilaya hiyo Sungwa Ndagambwene ni pamoja na mwakilishi wa madhehebu ya kidini,ofisi ya michezo,vijana na utamaduni,ofisi ya maendeleo ya jamii,mratibu wa CHF wilaya,meneja wa CHF kanda pamoja na mwakilishi wa mashirika ama vikundi vya wananchi.

Mkuu wa wilaya alisema kamati hiyo itaandaa utaratibu mzima wa jinsi gani hamasa ifanyike ili siku moja wilaya iwe sehemu ya zile zinazotolewa mifano kwa kufanya vizuri tofauti na sasa ambapo mwamko unaonekana mdogo.

Awali akizungumzia sababu za wananchi waliokuwa wamejiunga na mfuko huo kujitoa,mnganga mkuu wa wilaya alisema baadhi walikatishwa tama na kasoro zilizobainika ikiwemo uhaba wa dawa jambo ambalo alisema hivi sasa limewekewa mikakati tofauti na kipindi hicho.

Alisema tatizo jingine lililopunguza idadi ya wanachama wa mfuko ni kujitoa kwa Rungwe Smallholders Tea Growers Association (RSTGA) iliyokuwa akiwalipia wakulima wanachama wakati ikipata faida lakini baada ya kuyumba kwa uchumi wa dunia ikaelezwa hawapati tena faida.

No comments:

Post a Comment