Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, October 9, 2011

Kijiji kunufaika na uwekezaji


 
SERIKALI ya kijiji cha Luhanga wilaayani Mbarali imesisitiza kuwa uwekezaji wa kilimo unaolengwa kufanywa na Umoja wa wakulima wa Luhanga unalenga kuwanufaisha wakazi wa kijiji hicho na haupo kwa maslahi ya watu binafsi.

Uongozi wa kijiji hicho umesema makubaliano ya mkataba na umoja huo ni pamoja na umoja kutekeleza mambo makuu matatu ikiwemo kujenga ofisi ya kisasa ya kijiji,kuleta maji kijijini hapo kwaajili ya matumizi ya kilimo pamoja na kulipia ardhi waliyopewa kwaajili ya shughuli zao.

Mwenyekiti wa kijiji hicho Muhamed Msonsa alisema jana kuwa umoja huo utapaswa kulipa shilingi 5000 kwa kila hekari moja ya eneo walilopewa na kijiji hivyo kijiji kila mwaka kitakuwa kikikusanya jumla ya shilingi milioni 62 kwa hekari 5000 zilizotolewa.


Kwa upande wa afisa mtendaji wa kata ya Luhanga Aloyce Joseph alisema wapo wanasiasa wanaoonekana kuingilia kati uwekezaji huo na kuwalaghai wananchi kuwa kilichofanyika ni unyang’anyi wa ardhi hali ambayo imeonekana kuwagawa wanakijiji katika makundi.

Kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mbarali George Kagomba alisema uwekezaji wa Umoja huo utakinufaisha kijiji kwani kabla hata ya kuanza kwa shughuli husuika tayari umoja huo umeonesha nia kwa kuanza kuwasaidia wanakijiji kutatua changamoto mbalimbali.


No comments:

Post a Comment