Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, October 10, 2011

Kandiro-Jiulizeni mpo kufanya nini




MKUU WA mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amewataka madiwani na watendaji katika halmashauri za wilaya kila mmoja kujiuliza yupo katika nafasi yake kwaajili ipi.

Kandoro amesema kwa kufanya hivyo kila mmoja alipo ataweza kutambua wajibu wake na kuhakikisha anautekeleza akilenga kuyabadili maisha ya wananchi waliomwajiri.

Mkuu huyo wa mkoa,aliyasema hayo juzi(Oktoba 10) katika kikao maalumu cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Ileje kilicholenga kujadili taarifa ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa serikali CAG.

Alisema wapo baadhi ya madiwani na watendaji ambao wamekuwa wakiyasahau majukumu yao na kujikuta wanaendekeza siasa katika kila wanalofanya pasipo kutambua kuwa kufanya hivyo kunawacheleweshea maendeleo wananchi katika maeneo yao.

Aliwataka madiwani kuhakikisha wanakuwa na mshikamano katika kutafuta sukluhu za changamoto zinazowakabili wananchi badala ya kuendeleza makundi yaliyotokana na kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Kandoro alisema ushirikiano wa pamoja baina ya wadau hao kwa kushirikiana na wananchi ndio unaoweza kuongeza kipato cha mwananchi mmojammoja ambaye kwa mafanikio hayo ataweza kuuchangia uchumi wa wilaya hiyo na kuiondoa katika hali ya utegemezi wa asilimia 98 ya bajeti yake kutoka serikali kuu.

Alisema ni vema wadau hao wakaona aibu kwa halmashauri yao kuwa na uwezo wa kujitegemea kwa asilimia mbili pekee wakati ambao mkakati wa serikali ni kuona halmashauri zinajitegemea kwa asilimia 50.

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Glads Dyamvunye alisema ukosefu wa vyanzo vya mapato ni changamoto kubwa kwa halmashauri yake hali inayopelekea kuendelea kuwa tegemezi kwa serikali kuu.


No comments:

Post a Comment