Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, October 8, 2011

Mbunge Mbaroni


MBUNGE wa Mbarari Modestus Dickson Kilufi aliyekuwa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kutishia kuua atafikishwa mahakamani kesho jumatatu(Oktoba 10) na kwa sasa yupo nje kwa dhamana.

Mbunge Kilufi alikamatwa juzi(Oktoba 7) saa 10 jioni akiwa ofisini kwake ambapo kwa mujibu wa maelezo yake askari waliofika kumkamata ofisini hapo walimweliza kuwa alitishia kumuua ofisa mtendaji wa kata ya Ruiwa Jordan Masweve.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi alithibitisha kuachiwa kwa dhamana mbunge Kirufi alipozungumza na waandishi wa habari kwa njia ya simu.

Nyombi alisema mbunge huyo yupo nje kwa dhamana na atafikishwa mahakamani siku ya jumatatu kusomewa shitaka la kutishia kuua kwa maneno.

Hata hivyo kamanda huyo hakutaja mbunge atafikishwa katika mahakama ipi bali alisema ofisi ya mwanasheria wa serikali mfawidhi mkoa wa Mbeya ndiyo inayotambua mahakama hiyo kwani hata kukamatwa kwake kulilenga kutekeleza agizo la ofisi hiyo.

“Baada ya askari wetu kumkamata jana,leo hii tumemfikisha katika ofisi ya mwanasheria wa serikali na wao ndiyo watamfikisha mahakamani.Lakini hivi sasa yupo nje kwa dhamana na shitaka linalomkabili ni kutishia kuua kwa maneno” alisema Nyombi

Kwa upande wa Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Mbeya umesema hauhusiki na mashitaka yanayomkabili mbunge huyo kwani ni masuala yake binafsi na si ya chama.

Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Verena Shumbusho alisema jana kuwa shitaka la kutishia kuua linalomkabili mbunge kirufi chama hakiwezi kulitolea tamko lolote.

“Kama chama hatuwezi kutoa tamko lolote juu ya kukamatwa kwake wala shitaka linalomkabili.Hilo ni suala lake binafsi na chama hatulitambui kabisa” alisema Shumbusho.

No comments:

Post a Comment